Mzee wa tafakari

Friday, August 10, 2007




Powered By SeeBeforeYouDie.net
Share your Travel Experiance

Wednesday, August 08, 2007

CCM kumfia mikononi Rais Kikwete


WIKI hii Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ilifanya maamuzi mazito yakiwemo kuridhia kuwatimua madiwani watano wa chama hicho, kusimamisha viongozi wote wa Jumuiya ya Wazazi, maafisa wengine wa chama kutoka ofisi ndogo Lumumba jijini Dar es Salaam na Makao Makuu Dodoma.

Pia Kamati Kuu katika kikao chake kilichofanyika kuanzia Jumamosi hadi Jumatatu wiki hii, imetangaza kumvua haki ya
kuchaguliwa katika uongozi wa CCM, Thomas Nyimbo, baada ya kuthibitika kuwa tabia na mwenendo wake havifai.

Nyimbo alikuwa ni mmoja wa wagombea wa kiti cha uenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa. Hivi karibuni Nyimbo amekuwa akitoa shutuma nyingi dhidi ya mgombea wenzake.

Wengine waliosimamishwa uongozi na kamati hiyo ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi, Abiuod Maregesi, Makamu Mwenyekiti wa jumuiya hiyo,Ramadhan Suleiman Nzori, Babilas Mpemba na Katibu Mkuu, Cosmas Hinju, kwa tuhuma za kujihusisha na vitendo vya ubadhirifu wa fedha za jumuiya hiyo.

Mtu mwingine aliyekutana na makali ya panga la kamati hiyo ni Katibu wa CCM Mkoa wa Singida, Mujuni Kataraiya ambaye ametagazwa kufukuzwa kazi kutokana tuhuma za ubadhirifu wa mali za chama wakati alipokuwa Katibu wa chama hicho Mkoa wa Mwanza.

Kwa hakika maamuzi hayo ni mazito kwa chama hicho tawala kuwahi kuyatoa katika siku za hivi karibuni.

Swali tunalojiuliza hivi kweli CCM imeaamua kuzaliwa upya kutokana na kuamua kuanza kuchukua hatua za kuwashughulikia wabadhirifu wa mali zake au ni maamuzi ya kisiasa ambayo yamejifichia katika ubadhirifu?

Nasema hivyo kwa sababu kwa miaka yote CCM ndiyo ambayo ilikuwa chama ambacho kilisifika kutokana na kukumbatia ufisadi, hakuna hatua ambazo zimewahi kuchukuliwa kwa watu ambao wamehusika katika kuua miradi yake mikubwa ya uchumi.

Ilifikia mahali hata watumishi wa serikali waliokuwa wakifilisi mali za umma, badala ya kufukuzwa walipewa ulaji mwingine kwa kupewa mashirika mengine kuyaongoza. Kisa kanda wa CCM!

Leo kufumba na kufumbua tunaona CCM ile ile tuliyoizoea inaibuka na maamuzi mazito kama haya ya kuwatimua kazi wabadhirifu wa mali zake. Kwa hakika umetuachia maswali mengi ya kujiuliza.

Wapo wanaofikiria kuwa uamuzi wa kuwasimamisha viongozi wote wa jumuia ya wazazi ni wa kisiasa zaidi kutokana na juimuia hiyo viongozi wake hawakuwa kambi ya Rais Jakaya Kikwete wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2005.

Hisia zilizopo ni kwamba walioadhibiwa katika kikao hicho ni wale tu ambao walionekana kuwa hatari katika ustawi wa mtandao wa Rais Kikwete uliomwigiza madarakani.

Ingawa kamati kuu imetangaza rasmi kuvunja mtandao ndani ya chama hicho lakini ukweli unabaki pale pale kwamba wanaoendelea kumzunguka rais na kumpa ushauri ni wale wale wana mtandao ambao leo ndio wanaomshauri Rais vibaya katika uendeshaji wa uchumi na masuala mengine.

Lakini wana mtandao hao mbali ya kumzunguka rais lakini wana ajenda nyingine ya kutengeneza rais wa Tanzania wa baada ya rais Kikwete kumaliza muda wake.

Dhambi kubwa ambayo imewaponza watu hao walioadhibiwa ni kuwa na mtizamo toafuti ndani ya chama hicho. Ingawa hao wameadhibiwa lakini hiyo imetumika kama njia yakuwatisha wengine ambao wanaonekana kuwa tishjiop la mtandao huo.

Miongoni mwa watu ambao mpaka sasa wanaonekana kukigawa chama kutokana na nguvu walizonazo ambao sio wana mtandao ni pamoja na Waziri wa Nchi ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Profesa Mark Mwandosya, waziri mkuu wa zamani, Frederick Sumaye, na waziri wa ardhi na maendeleo ya makazi, John Magufuli.

Kwa hakika nyufa ndani ya CCM bado ni kubwa na kwamba kama hatua za kumaliza makundi ndani ya chama hicho hazitachukuliwa haraka, huenda chama hicho kikamfia mikononi Rais Kikwete kama ataendelea kulea kundi la marafiki zake la wanamtandao.

Wednesday, August 01, 2007

Vitambi vya ukimwi

WIKI hii serikali ilianzisha kampeni maalumu ya
upimaji wa hiyari kujua kama wananchi wameambukizwa
virusi vya ukimwi iliyoongozwa na Rais Jakaya Kikwete
ambaye yeye na mkewe, Salma walipima jijini Dar es
Salaam wakiungwa mkono na mamia ya wakazi
waliojitokeza.

Kampeni hiyo pia ina lengo kuanza kutoa dawa za
kupunguza makali ya ugonjwa huo (ARVs) bure kwa watu
watakaobainika kuwa wameathirika.

Mara baada ya kupima, Rais Kikwete alionyesha majibu
yake dharani ikionyesha kuwa yuko safi na mkewe na
baadhi ya wanasiasa waliopima siku hiyo baadhi yao
walitangaza majibu yao huku wengine wakikaa kimya.
Wengine walikimbia kujitokeza kupima.

Kampeni hiyo ya kupima kwa hiari sasa imeanza kuchukua
sura ya kisiasa zaidi, wengi hasa viongozi wanaotoka
chama tawala wanataka kujitokeza kupima ili
kumwonyesha Rais kwamba wako pamoja naye.

Lakini inawezekana kwamba viongozi wapinzani,
wanajitokeza kupima ili kupata imani ya wananchi kuwa
wako fiti kwa ajili ya kugombea urais katika uchaguzi
ujao.

Wakati kampeni hiyo ikiendelea, baadhi ya wabunge wa
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati
wakichangia hotuba ya makadirio ya matumizi ya Wizara
ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa mwaka wa fedha 2007/8
bungeni Dodoma wameungana na waathirika wa ukimwi
kueleza wasiwasi wao kuhusu udaganyifu uliopo katika
ARVs.

Wabunge wanasema kuwa baadhi ya dawa za ARVs
zimeelezwa kwamba zinasababisha madhara kwa watu
wanaozitumia.

Kwa kifupi ni kwamba fedha kwa ajili ya kununulia dawa
za ARVs zinadaiwa kutumiwa kwa matumizi mengine na
nyingine kuishia kunenepesha matumbo ya wakubwa wa
serikali.

Kutokana na ufisadi mkubwa uliopo katika fedha
zinazotoka kwa wahisani hususan mfuko wa kusaidia
wenye ukimwi (Global Fund), waathirika wanapewa ARVs
ambazo zimekwisha muda wa matumizi yake na nyingine
ambazo haziwapi madhara makubwa.

Baadhi ya dawa hizo zinadaiwa kusababishia athari
mbalimbali watumiaji ikiwamo kukua matiti na makalio,
kuathiri mwenendo wa kula na kuwafanya wawe na matumbo
makubwa kiasi kwamba wanawake huonekana kama
wajawazito na wakati mwingine huwaongezea hamu ya
kushiriki vitendo vya ngono.

Kwa hakika malalamiko haya ni mazito ambayo serikali
inapaswa kuyatolea maelezo ya kina ili wananchi wajue.


Si wabunge wenye hofu kuhusiana na malalamiko hayo,
bali wananchi wote wanataka kujua serikali
imeshushghulikia vipi tatizo hilo na watu wanaokula
fedha za ukimwi.

Ninasema hivyo kwa kutambua jinsi matumizi ya ARV
yalivyo tete na kwa kuzingatia kwamba mtumiaji
anapaswa azitumie kwa maisha yake yote huku
akizingatia masharti na ushauri wa madaktari kuhusu
aina ya vyakula na dawa za kutumia.

Katika mazingira kama hayo mategemeo makubwa ya
mwathirika ni katika matumizi ya ARVs sahihi. Iwapo
ARVs hizo zinaleta madhara, ni wazi kwamba serikali
inawaandalia vifo vya haraka watu hao bila wasiwasi.

Ni vyema sasa kwa Serikali kusikiliza kilio hicho na
kutoa maelekezo sahihi kabla watumiaji hawajaingiwa
woga na kuacha kuzitumia, kama baadhi yao
walivyotishia.

CCM kumfia mikononi Rais Kikwete


WIKI hii Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ilifanya maamuzi mazito yakiwemo kuridhia kuwatimua madiwani watano wa chama hicho, kusimamisha viongozi wote wa Jumuiya ya Wazazi, maafisa wengine wa chama kutoka ofisi ndogo Lumumba jijini Dar es Salaam na Makao Makuu Dodoma.

Pia Kamati Kuu katika kikao chake kilichofanyika kuanzia Jumamosi hadi Jumatatu wiki hii, imetangaza kumvua haki ya
kuchaguliwa katika uongozi wa CCM, Thomas Nyimbo, baada ya kuthibitika kuwa tabia na mwenendo wake havifai.

Nyimbo alikuwa ni mmoja wa wagombea wa kiti cha uenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa. Hivi karibuni Nyimbo amekuwa akitoa shutuma nyingi dhidi ya mgombea wenzake.

Wengine waliosimamishwa uongozi na kamati hiyo ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi, Abiuod Maregesi, Makamu Mwenyekiti wa jumuiya hiyo,Ramadhan Suleiman Nzori, Babilas Mpemba na Katibu Mkuu, Cosmas Hinju, kwa tuhuma za kujihusisha na vitendo vya ubadhirifu wa fedha za jumuiya hiyo.

Mtu mwingine aliyekutana na makali ya panga la kamati hiyo ni Katibu wa CCM Mkoa wa Singida, Mujuni Kataraiya ambaye ametagazwa kufukuzwa kazi kutokana tuhuma za ubadhirifu wa mali za chama wakati alipokuwa Katibu wa chama hicho Mkoa wa Mwanza.

Kwa hakika maamuzi hayo ni mazito kwa chama hicho tawala kuwahi kuyatoa katika siku za hivi karibuni.

Swali tunalojiuliza hivi kweli CCM imeaamua kuzaliwa upya kutokana na kuamua kuanza kuchukua hatua za kuwashughulikia wabadhirifu wa mali zake au ni maamuzi ya kisiasa ambayo yamejifichia katika ubadhirifu?

Nasema hivyo kwa sababu kwa miaka yote CCM ndiyo ambayo ilikuwa chama ambacho kilisifika kutokana na kukumbatia ufisadi, hakuna hatua ambazo zimewahi kuchukuliwa kwa watu ambao wamehusika katika kuua miradi yake mikubwa ya uchumi.

Ilifikia mahali hata watumishi wa serikali waliokuwa wakifilisi mali za umma, badala ya kufukuzwa walipewa ulaji mwingine kwa kupewa mashirika mengine kuyaongoza. Kisa kanda wa CCM!

Leo kufumba na kufumbua tunaona CCM ile ile tuliyoizoea inaibuka na maamuzi mazito kama haya ya kuwatimua kazi wabadhirifu wa mali zake. Kwa hakika umetuachia maswali mengi ya kujiuliza.

Wapo wanaofikiria kuwa uamuzi wa kuwasimamisha viongozi wote wa jumuia ya wazazi ni wa kisiasa zaidi kutokana na juimuia hiyo viongozi wake hawakuwa kambi ya Rais Jakaya Kikwete wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2005.

Hisia zilizopo ni kwamba walioadhibiwa katika kikao hicho ni wale tu ambao walionekana kuwa hatari katika ustawi wa mtandao wa Rais Kikwete uliomwigiza madarakani.

Ingawa kamati kuu imetangaza rasmi kuvunja mtandao ndani ya chama hicho lakini ukweli unabaki pale pale kwamba wanaoendelea kumzunguka rais na kumpa ushauri ni wale wale wana mtandao ambao leo ndio wanaomshauri Rais vibaya katika uendeshaji wa uchumi na masuala mengine.

Lakini wana mtandao hao mbali ya kumzunguka rais lakini wana ajenda nyingine ya kutengeneza rais wa Tanzania wa baada ya rais Kikwete kumaliza muda wake.

Dhambi kubwa ambayo imewaponza watu hao walioadhibiwa ni kuwa na mtizamo toafuti ndani ya chama hicho. Ingawa hao wameadhibiwa lakini hiyo imetumika kama njia yakuwatisha wengine ambao wanaonekana kuwa tishjiop la mtandao huo.

Miongoni mwa watu ambao mpaka sasa wanaonekana kukigawa chama kutokana na nguvu walizonazo ambao sio wana mtandao ni pamoja na Waziri wa Nchi ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Profesa Mark Mwandosya, waziri mkuu wa zamani, Frederick Sumaye, na waziri wa ardhi na maendeleo ya makazi, John Magufuli.

Kwa hakika nyufa ndani ya CCM bado ni kubwa na kwamba kama hatua za kumaliza makundi ndani ya chama hicho hazitachukuliwa haraka, huenda chama hicho kikamfia mikononi Rais Kikwete kama ataendelea kulea kundi la marafiki zake la wanamtandao.

Wednesday, February 07, 2007

Tuesday, February 06, 2007

Mawaziri watakaoshindwa kumudu kasi mpya watimuliwe mapema


JUZI Rais Jakaya Kikwete aliteua baraza lake la kwanza la mawaziri, likiwa idadi ya mawaziri 60 kati yao 40 ni wapya na 20 ni wale waliokuwa katika baraza lililopita.

Hata hivyo, Rais Kikwete wakati akitangaza baraza hilo alisema kuwa wakati analiunda amezingatia agenda na majukumu yaliyopo mbele ya serikali hiyo.

Pia Rais Kikwete alisema sababu nyingine ambayo imefanya baraza hilo kuwa katika muundo huo ni pamoja na kunzingatia uwakilishi na umoja wa kitaifa.

Kutokana na muundo wa baraza hilo kuwa kujumuisha mawaziri wengi angalau kila mkoa umepata waziri mmoja.

Kikwete pia akavunja baadhi ya wizara na kuziunganisha pamoja na kuunda wizara mpya kadhaa. Mbali ya kuongeza wizara pia manaibu waziri katika wizara nyingine wameongezwa idadi.

Kama alivyosema yote hayo ameyafanya kwa nia ya kuuleta ufanisi na kuwatatulia matatizo wananchi kwa njia ambayo ni rahisi zaidi.

Kwa hilo tunakubaliana nalo kwa asilimia mia moja kwa sababu Watanzania kwa muda mrefu wamekuwa wakikerwa na mambo mengi bila ya kupatiwa ufumbuzi.

Hata hivyo, pamoja na nia njema ya Rais Kikwete kuweka mfumo mpya wa baraza la mawaziri, lakini kuwa na mawaziri wengi kunaweza kuongeza matumizi ya serikali.

Hakuna ambaye anaweza kusimama kupinga kuwa matumizi ya serikali yataongezeka kutokana na kila waziri kuhitaji kupatiwa mahitaji muhimu kutokana wadhifa wao ikiwamo kuwa kuishi katika nyumba ya serikali, gari ya kifaharai maarufu 'shangingi' na matumizi mengine ya kila siku.

Matumizi ya sasa ya serikali kwa kiasi kikubwa yanakwenda kwenye shughuli za utawala, hivyo kuongeza idadi ya wizara na idadi ya mawaziri ni wazi kuwa unawafanya watanzania wajikamue zaidi mifukoni kulipa kodi ili waweze kufidia gharama za uendeshaji za mawaziri.

Si vyema kwa sasa kushauri kupunguza idadi ya mawaziri na wizara hizo kutokana ukweli kuwa rais tayari ameshawateua mawaziri hao na kuwaapisha tayari kwa kuingia kazini.Ila kinachotakiwa hatua kadhaa za kupunguza matumizi ya mawaziri hao zichukuliwe haraka.

Moja ya eneo ambalo ni wazi linaonekena kuwa linachukua matumizi makubwa katika uendeshaji wa serikali ni magari ya fahari wanayotumia mawaziri na wakuu wa idara za serikali.

Gazeti hili lilishawahi kuandika huko nyuma kuwa serikali inatumia fedha nyingi kwa ajili ya kugharimia magari ya kifahari ya mawaziri na watumishi wengine wa serikali.

Ni wazi kuwa kama gharama hizo zitaachwa bila ya kupunguzwa ukitilia amaanani kuwa idadi ya mawaziri 20 wameongezeka tutaendelea kubeba mzigo mzito mkubwa amabo huenda mbele ya safari itatupunguzia kasi yetu ya kuelekea katika maendeleo ikapungua.

Ni vyema sasa tuukajiuliza kwa nini tuendelee kubeba gharama hizi? Kwa nini tusizipunguze kwa kubadilisha aina ya magari wanayotumia mawaziri? Hivi mawaziri wakitumia magari ya kawaida hawatakuwa hadhi ya kuitwa mawaziri? Nadhani hilo linawezekana kabisa kwa kuwapa mawaziri na wakuu wengine wa idara za serikali magari ya kawaida.

Kuna nchi nyingi zimeliona hilo na kuamua kupunguza gharama za uendeshaji wa magari ya serikali kwa watumishi wake kuacha kutumia magari ya kifahari na kutumia ya kawaida.

Burundi ni mfano wa nchi hizo ambayo hivi sasa imeamua watumishi wake wakiwamo mawaziri kutumia magari ya kawaida.

Kama serikali itaamua kuacha kutumia magari hayo ambayo yanatumia mafuta mengi na vipuri vyake ni gari, serikali inaweza kudhibiti kuongezeka kwa gharama za uendeshaji wa ofisi mawaziri.

Hakuna mtu ambaye anaweza kupigana na dhamira ya Rais Kikwete ya kuweza kuwaletea maisha bora, kinachotakiwa ni kuaangalia namna ya kupunguza matumizi.

Kwa upande wao mawaziri walioteuliwa, Rais Kikwete awape mikataba ambayo itawafanya wawajibike na kuwafanya waondokewe na ndoto kuwa sasa wameingia katika neema ya kuishi maisha ya peponi ya kupata kila wanachohitaji hata kama kwa njia ya kuwabia wananchi.

Waziri atakayeshindwa kutimiza malengo yake aliyopangiwa basi aondolewe mara moja badala ya kumhamishia sehemu nyingine au kumwacha kwa muda mrefu akiboronga. Muda wa kufanya kazi kirafiki haupo tena katika karne hii.

Naugana na kauli ya Rais Kikwete aliyoitoa mara baada ya kutanagaza baraza la mawaziri Ikulu jijini Dar es Salaam kuwa ataanza kukutana mawaziri mmoja mmoja akiwa na watumishi wa wizara aliyopewa kuwapa majukumu.

Nadhani hiyo ndiyo njia pekee itakayowafanya wawajibike kuwatumia wananchi kwa kuwaletea maisha bora. watanzania tunahitaji mawaziri wachapakazi sio wabababishaji ambao watatumie fedha zetu za kodi kuwalipa mishahara na malupulupu mengine bila ya kuona wanachofanya.

Kificho na mtego wa panya

WIKI hii Spika wa Baraza la Wawakilishi, Pandu Ameir Kificho alimzuia waziri Kivuli wa Fedha na Uchumi kupiti Chama cha Wananchi (CUF), Abasi Muhunzi, kutoa hotuba yake kabla ya kuiwasilisha kwake kwa madia ni utekelezaji wa kanuni za Baraza.

Kificho bila ya kuficha alisema agizo lake la kutaka kuziona bajeti za wapinzani kabla hazijawasilishwa barazani litaendelea kuwako na kamwe Baraza lake halitastahimili kauli za matuzi na kejeli. 
Alisema kumekuwako na vitendo visivyovumilika vinavyofanywa na mawaziri kivuli vikiwamo kutoa lugha za kebehi zinazokwenda kinyume cha kanuni.

Alinukuu kanuni ya 151 inayosema kama kutatokea mambo ambayo kanuni yetu haikusema, basi Spika ndio mlezi mkuu wa kanuni zetu, ingawa kanuni hizi ni mali ya wajumbe wote,” alisema Spika Kificho.
Kwa hakika kitendoi hicho kimenikumbusha hadithi ya mfalme na mtego wa panya.
Msomaji wangu sio vibaya nikieleza kwa kifupi hadithi hii ambayo inafanana sana na mamabo ambayo yanafanyika zanzibar kwa sasa.

Mfalme Siku nyingi alikuwa mkulima mzuri wa mahindi na mazo mengine ya nafaka.
Kila mwaka alivuna mazo mengi na kuyahifadhi katika ghala kubwa nyumbani kwake. Kutokana na ukulima huoalisifika sana katika katika eneo lake.

Hata hivyo, alikuwa na amatataizo kadha aambayo yalikuwa yanamsumbua. Mojawapo lilikuwa ni panya wengi waliokuwa wakila nafaka zake ghalani.

Baadaye panya kumsumbua kwa muda mrefu aliamua kutafuta mtego wa kuwanasa. Mtego huo aliuweka mahali ambako palikuwa ndio njia ya panya kuingia ghalani.

Panya kama kawaida yao walipoamua kwenda kula nafalaka ghalani walikuta mtego ambao walishitukia na kuamua kwenda kutafuta chakula sehemu nyingine.

Hata hivyo pamoja na kuamua kwenda kutafuta chakula sehemu nyingine waliamua kuwaambia wanyama wengine waliokuwa wakifungwa na mfalme kama vile bata , paka, mbuzi na farasi kuwa wautegeua mtego huo kwa vile unaweza kuwanasa.
Mtengo huo baada ya siku tatu ulimnasa nyoka. Mfalme aliposikia kuwa mtego umenasa akaajua mbaya wake panya atakuwa amesaswa alifurahi na kwenda kumwangalia.

Alipofika karibu na mtego huo aliumwa na nyoka huyo ambaye baadaye aliumwa na kufariki dunia.
Baada ya kufariki mbuzi na bata walichinjwa kuwapatia chakula watu waliofika msibani na farasi akabaki mbeba mzigo huku panya akibaki hana chakula kutokana na familia hiyo kusambaratika baada ya kifo cha mfalme.

Baada ya tukio hilo, panya akawacheka wabnyama wenzake kuwa kama wangemsikiliza na kuutegua mtego huo hawangepata shida na wengine kuchijwa.

Hadithi hii inafanana sana vitendo vya ubaguzi na uchohezi ambavyo vianza kufanywa ambayo kama havitazuiwa ni wazi mambo makubwa yanaweza kutokea
Kitendo cha Spika Kificho kudai hotuba za wapinzani azipitie kwanza ni mwanzo wa chokochoko wa hali iliayoanza kutulia visiwani.

Sioni sababu iliyomfanya Kificho kuamua kudai kwanza kuziona hotuba zao wakati hakuna kigezo kama hicho wakati wanapochangia hoja zao bungeni.

Mbunge ni mtu mzima ambaye anajua wajibu wake hawezi kuzungumza maneno ya kejeli na au kutukana wakati akijua wazi kuwa kuna kanuni ambazo zinambana kufanya hivyo.

Kificho anapaswa kusimamia kanuni zote za Baraza hilo na kuwaacha wapinzani wawe huru kutoa mawazo yao ya upinzani bila ya kuwasilishwa kwake kwanza.

Msimamo huo wa Spika unaonekana wazi kuwa sasa jahazi la zanzibar ambalo lilikuwa liyumba kwa muda mrefu lianza kukaa sawa majini analitoboa ili lizame.

Kwa hakika kama chokochoko zinazofanywa na kificho dhidi ya wawakilishi wa CUF kama hazitazuiwa mapema basi, matatizo makubwa yatatokea.

Karume kubali serikali ya mseto yaishe!

UCHAGUZI wa rais, wabunge na masheha visiwani Zanzibar uliofanyika Jumapili iliyopita ulifikia ukingoni Jumanne wiki hii baada ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) kumtangaza Rais Aman Karume kuwa ndiye mshindi wa kiti cha urais.

Kwa mujibu wa ZEC, Karume alishinda kwa asilimia 53.2 akiwa mbele ya mgombea wa Chama cha Wananchi (CUF), Seif Sharrif Hamad aliyepata asilimia 46.1 ya kura zote zilizopigwa.

Karume aliapishwa asubuhi ya siku hiyo katika sherehe zilizohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali ya Muungano na baadhi za mabalozi zilizopo hapa nchini.

Hata hivyo, uchaguzi huo, ulitawaliwa na dosari kadhaa zikiwamo za baadhi ya wapigakura kushindwa kuona majina yao vituoni, baadhi ya vituo kuchelewa kufunguliwa na baadhi ya watu kugundulika kuwa walitaka kupiga kura mara mbili.

Tayari Marekani imesema haijafikia uamuzi wa kukubali kuwa uchaguzi wa Zanzibar ulikuwa huru na haki, mpaka tuhuma zilizojitokeza za ukiukwaji mkubwa wa taratibu za kupiga kura zitakapofafanuliwa.

Taarifa ya ubalozi wa Marekani kwa vyombo vya habari, nchi hiyo imesema haikuhudhuria sherehe za kuapishwa kwa Rais Karume kwa sababu kuna mambo ambayo hajawekwa wazi kuhusu uchaguzi huo.

Ubalozi huo umesema kwamba ingawa wanapongeza uboreshaji ulioonekana katika mchakato mzima wa uchaguzi wa Zanzibar, ukilinganishwa na ule uliokuwapo wakati wa uchaguzi wa 2000.

Bado wanatiwa mashaka na ukiukwaji mkubwa ulioshuhudiwa na waangalizi wa kimataifa, ikiwamo taasisi ya National Democratic Institute (NDI).

Kutokana na hali hiyo, Marekani imejitoa katika kundi la nchi na taasisi zilizotoa tamko kuwa uchaguzi huo ulikuwa huru na wa haki.

Hata hivyo, kwa upande wake Serikali ya mapinduzi Zanzibar imepinga vikali taarifa hiyo kwa maelezo kuwa kama waangalizi wote wa nje wamesema ulikuwa huru na haki iweje kwa iwe kwa Marekani tu. Wameitaka serikali ya Marekani kuacha kungilia masulaa ya ndani ya Zanzibar.

Sio nia yangu leo katika safu hii kuangalia dosari zilizojitokeza ila ninachotaka kuzungumzia ni suala la serikali ya umoja.

Baada ya Rais Karume kuapishwa alifanya mkutano na waandishi wa habari na kueleza wazi msimamo wake kuwa hayupo tayari hivi sasa kuunda serikali ya mseto ambayo inawashirikisha CUF.

Karume bila ya kusita alisema katika utawala wake hana wazo la kuunda serikali ya mseto kwa kushirikisha watu kutoka vyama vya upinzani.

Kwa hakika kauli hiyo ya Karume inazusha maswali mengi ya kujiuliza iwapo kiongozi huyo ameyasema hayo dhati kutoka katika sakafu ya moyo wake au la!.

Inaniwia vigumu kuamini kuwa Karume alisema hayo kwa dhati kutokana na hali tete ya Zanzibar ilivyo hivi sasa.

Suala la serikali ya mseto haliwezi kukwepeka kutokana na wapinzani kupata kura nyingi. Kuwaacha nje ya karibu nusu ya wazanzibari katika utawala ni kuendelea kuzusha migogoro isiyofaa.

Najua kuwa Maalim Seif tayari amekataa kuyatambua matokeo ya uchaguzi kwa madai kuwa chama chake ndicho kilichoshinda katika uchaguzi huo, lakini hiyo haikuwa sababu ya Karume kuwa na msimamo ambao unaonyesha kuendeleza ufa miongoni mwa wazazibari.

Kudharau wapinzania ambao wamepata asilimia 46.1 ya kura zote zilizopigwa ni kuwadharu karibu nusu ya wazanazibari ambao waliwapigia kura wapinzania.

Ubinafsisi wa kung'angnia madaraka katika enzi hizi iumepitwa na wakati. kinachotakiwa kufanyika hivi sasa kwa Karume ni kukubali kuunda serikali ya mseto ili kumaliza matatizo ya mgawanyiko yaliyopo hivi sasa visiwani humo.

Ushauri wa serikali ya mapinduzi Zanzibar kuunda serikali itakayowashirikisha wapinzani umeanza kutolewa siku nyingi na watu mbalimbali wakiwamo Marehemu Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere.

Mwalimu Nyerere baada ya uchaguzi wa 1995 alimshauri Rais Salmin Amour aunde serikali ya mseto lakini hakusikiliza ushauri huo, hali ambayo iliendeleza migogoro mingi ya kisiasa.

Vile vile, wapo watu mbalimbali ambao wamekuwa wakishauri kuwepo kwa serikali ya mseto lakini inaonekana suala hilo kwa watalawa wanaoigia madarakani hawataki kulisikia hali ambayo ndio imekuwa chanzo cha matatizo mengi yalizoaa mwafaka wa CCM na CUF.

Kutokana na Karume kutangaza rasimi msimamo wake mapema, kinachoonekana ni kuwa visiwa hivyo vitaendelea kuwa na vurugu huenda mwafaka wa tatu kati ya CCM na CUF ukasainiwa tena.

Karume mtaingia mwafaka mara ngapi? kubali yaishe.

Sarungi hapo umepotoka

Profesa Philemon Sarungi amejizolea sifa na heshima nyingi kwa Watanzania kutokana na rekodi yake ya utumishi katika nyadhifa mbalimbali hapa nchini.

Sarungi ambaye ni Daktari bingwa wa mifupa anakumbukwa sana na Watanzania kutokana na mara kwa mara kurejea chumba cha upasuaji hospitalini kuhudumia wagonjwa kila bila ya kujali nyadhifa alizo nazo za ubunge na uwaziri.

Katika majanga makubwa ya kitaifa mchango wake mkubwa huonekana zaidi. Wakati huo huvaa nguo rasmi za utatibu na kuwashiriki bega kwa bega na madaktari wengine kuokoa maisha ya majeruhi.

Kwa hakika Profesa Sarungi ameonyesha jinsi ambavyo Watanzania wanatakiwa kuzitumia taaluma zao vyema katika kuwasaidia wenzao bila ya kuangalia kwamba hivi sasa wanafanya kazi zipi.

Hata hivyo, hivi karibuni utumishi mzuri wa Waziri huyu msomi aliyebobea ameanza kuupaka matope baada ya kutoa kauli bungeni ambayo inaonyesha dhahiri kuwa sasa anataka kutugoganisha raia askari wetu.

Kauli ya Waziri Sarungi ambayo nitazungumzia katika safu hii leo ni ile ambayo kuwaonya raia kuacha kuwachokoza askari wa majeshi yetu kwa namna yoyote ikiwamo kuwachukulia wake zao.

Sarungi alikaririwa akiwaasa wananchi kuwa wakiwachokoza kwa kuwatolea maneno yasiyofaa au kuwachukuliwa wakeza zao, wajue kuwa ugomvi wa askari mmoja huwa askari wote.

Kitu cha kushangaza katika kauli yake Sarungi alisahau kutuleza iwapo askari atamchukua mke wa raia yeye atafanywe nini?

Sarungi tunamheshimu Watanzania kama nilivyoeleza hapo awali, lakini kitendo cha kutoa kauli kama hiyo kinatushangaza.

Tunakubali kuwa raia hawapaswi kuwachokoza askari wetu kwa namna yoyote kwa sababu kwa kufanya hivyo ni kuvunja sheria za nchi, lakini kwa sababu nchi hii inaendeshwa kwa sheria na utawala bora pia hatutarajii askari kutoka jeshi lolote nchini akavamia raia na kufanya uchokozi.

Kwasababu tuna matukio kadhaa ambayo yametokea hapa nchini ya askari kuanzisha ugomvi dhidi ya raia na kwamba baada ya uchunguzi baadhi yao wengine wamefukuzwa kazi.

Kinachotisha ni kuwa kauli ya Sarungi hakugusia kuwaonya askari kama vile raia ni halali kuwafanyiwa vurugu.

Kwa vile, Watanzania sio utamaduni wetu wa kuwa na vurugu, tunaishi kwa kupendana na kuheshimiana, basi sheria ifuatwe kwa pande zote kama raia atamchokoza askari achukuliwe hatua za kisheria na hivyo hivyo kwa askari akimchokoza askari achukuliwe hatua za kisheria.

Kutoa kauli ya upande mmoja inaweza kuhamasisha baadhi ya askari kuhisi kuwa sasa wameruhusiwa kujichukulia sheria mkononi kuwaadhibu raia.

Kwa nchi ya amani inayofuata utawala wa sheria kama Tanzania hatuamini kama tumefikia mahali ambako tunashindwa kuishi na askari wetu kwa amani hadi kufikia mahali waziri kutoa kauli kama hiyo.

Moja ya majeshi ambayo yanasifika kwa askari wake kuwa na nidhamu duniani basi ni majeshi yetu ya Tanzania. Kutokana na kuwa na sifa hiyo ninaamini kuwa ni baadhi ya askari wachache ambao wamekuwa wakijiingiza katika ugomvi na raia.

Tunaamini ili kuondoa tatizo hili, basi sheria ichukue mkondo wake bila ya kubagua huyu ni nani na yule ni nani.

Nguvu za soda za serikali kuhusu wamachinga

KAMA kuna kitu ambacho watanzania sasa wamekingundua ni jinsi serikali yao inavyoendesha mambo yake kwa mtindo wa zima moto.

Wameshaelewa kuwa kama kuna amri itatolewa na viongozi wa juu wa serikali, basi amri huyo ni ya kupita tu, mara nyingi huwa hakuna ufuatiliaji wa karibu.

Sijui ni watendaji wa viongozi hawa ndio wanaowakwamisha ama ni viongozi wenyewe wanatoa maagizo mengi mno kiasi kwamba mengine wanajikuta hawayakumbuki tena. Ama maagizo haya yanatolewa tu kwa sababu viongozi hawa wanataka kuonyeshwa kwamba wanafanya kazi.

Kwa hakika hakuna majibu mwafaka ambayo yanaweza kupatikana kwa urahisi labda tu viongozi hawa watuambie.

Kilichgonisukuma kuandika mambo haya ni ukweli ulianza kujionyesha katika kushindwa kwa agizo la wamachinga tu la kuwaweka katika maeneo maalum waliyopangiwa jijini Dar es salaam.

Operesheni ya kusafisha jiji la Dar es Salam iliyoendeshwa Oktoba mwaka jana, ilifanikisha kuwaondoa wafanyabiashara ndogo ndogo maarufu kwa jina la wamachinga katika maeneo yasiyoruhusiwa kuendesha shughuli zao.

Pia waliokuwa wamejenga maduka, vibanda na aina zote za majengo kwenye maeneo ya barabara, nao walivunjiwa. Hatua hii ilipendezesha jiji la Dar es Salaam kwa kiwango cha juu kabisa ambacho kwa mingi iliyopita hali hiyo haijawahi kufikiwa.

Operesheni hii ilisimamiwa kikamilifu na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Abbas Kandoro, ambaye alikuwa akitekeleza maagizo ya Rais jakaya Kikwete na kupitia kwa waziri Mkuu, Edward Lowassa.

Baada ya hatua hiyo, mgambo pamoja na askari polisi walimwagwa kila mtaaa kuhakikisha kuwa hakuna mmachinga ambaye anarejea katika maeneo hayo tena.

Mbali ya kumwagwa askari mitaani pia tulishuhudia viongozi karibu wote wa serikali wakitoa maagizo na tambo nyingi kwamba chinga hawatarejea katika maeneo hayo kamwe. Tukasikia kitu kingine kwamba ili kuwafanya wamachinga wafanyie shughuli zao katika eneo lililo bora jengo la kisasa linajengwa Karume.

Waziri mkuu Lowassa alienda mbali zaidi ya kuagiza manispaa za jiji kuanzisha bustani katika maeneo ambayo yaliyokuwa yakitumkiwa na wamachinga, lakini hata hilo halijafanyika.

Yakaisha tukasubiri kuona utekelezaji wake, lakini kama ilivyo kawaida kwa maagizo mengi ya serikali ambayo huwa hayachelewi kupuuzwa , taratibu tulianza kuona mmachinga mmoja mmoja anarejea mitaani na sasa wamejazana tena kama zamani.

Wengine hivi sasa wapo katika harakati za kuanza kujenga vibanda katika maeneo yale yale waliyondolewa, serikali ipo, haichukui hatua. hii inoanekana kama vile juhudi zilizofanyika kuhawamisha zilikuwa sawa na nguvu za soda aina ya coca cola ambayo hufoka mara ikifunguliwa baada ya muda inatulia.

Ni wazi kuwa kazi hii si nyepesi hasa kutokana na usugu uliojengwa na wamachinga kwa miaka mingi kwamba wana haki ya kuvunja sheria na hakuna watakalofanyiwa na vyombo vyenye mamlaka ya kusimamia miji yetu.

Nenda hivi sasa katika mitaa ya Kariakoo – mzunguko wa shule ya Uhuru, Kariakoo Sokoni na mtaa wa Msimbazi, Tandamti, Pemba Ubungo stendi ya daladala hapa nataja kwa uchache tu, bishara wa wamachinga inaendelea kama kawaida.

Wamachinga wanaodai kuwa maeneo waliyopangiwa hayana biashara na kwamba hata miundombinu haipo kama vile stendi ya mabasi ambayo huwa ni kigezo kikubwa cha kupata wateja. Wamachinga wanaolalamika haya ni wale ambao wapo katika soko la Kigogosambusa.

Ni wazi kuwa sulala la wamachinga sasa serikali ya awamu ya nne inapaswa kuonyeshwa kwamba, maagizo ya serikali sio ya kuchezewa ovyo voyo kwamba inapotoa maagizo yake yanapaswa kutekelezwa.

Awamu ya nne imekwisha kutagaza wazi azima yake ya kuhakikisha kuwa inatekeleza mambo yake kwa kasi na kufuata sheria na kwamba watedaji ambao watashindwa kutekeleaza maagizo ya viongozi wa juu watafukuzwa kazi.

Tunaasubiri kuona suala hili la wamachinga kujua ni nani ambaye amezembea mpaka kusababisha watu hawa wakatoka katika maeneo waliyopngiwa na kurejea mitaani kufanya shughuli zao.

Kandoro ambaye ameonyesha kuwa anauwezo wa kuongoza mkoa wa Dar es Salaam tangu aingie, tunadhani hili la wamachinga kurejea mitaani litakuwa ni mtihani wake mwingine kuonyesha kuwa anaweza kusimamia maagizo ya wakubwa wake barabara.

Kushindwa kwa suala hili ni aibu kwa rais Kakaya Kikwete na waziri mkuu wake Lowassa ambao sulala hili tangu waingie madarakani mwaka mmoja uliopita wamelivalia njunga. Pia itakuwa ni kuonyesha kuwa sasa serikali yao imekwama kutekeleza maamuzi yake yenyewe.

Wanaohujumu miundombinu ya maji ni watanzania?

WIKI iliyopita Mahakama ya mwanzo ya Manzese iliwahukumu wakazi wawili wa jijini Dar es Salaam kwenda jela miaka mitano kila mmoja kwa wizi wa mali ya Shirika la Uendeshaji la Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASCO) yenye thamani ya sh milioni 1.5.

Watu hao wamefungwa baada ya kupatikana na kosa la wizi wa vifaa vya air valve, washout tatu na mita ya maji.

Katika hukumu yake hakimu mfawidhi Mariam Masamalu alisema anatoa adhabu hiyo kali kwa washitakiwa ili iwe fundisho kwa watu wengine ambao wamekuwa na tabia ya kuhujumua miundo mbiunu ya maji nchini na kwamba mara baada ya kumaliza kifungo gerezani itabidi warejeshe thamani ya mali ya DAWASCO.

Kwa hakika, hukumu hiyo imesaidia kuwakumbusha watanzania wenye mazoea ya kuhujumu miumdo mbinu ya maira ya maendeleo kuwa serikali ina mikono mirefu na kwamba haijalala.

Vitendo vya kuhujumu miundombinu ya miradi ya maendeleo ikiwamo ya DAWASCO imekuwa kawaida kwa baadhi ya watanzania.

Baadhi ya watu wanadiriki hata kukata nyaya za umeme zenye moto na wengine wanajiunganishia maji kwenye bomba kuu na kuiba mita za maji bila ya kujali kwa kufanya hivyo ni kuzipunguzia mamlaka zinazohusika uwezo wa kutoa huduma kwa wananchi.

Sio siku nyingi vyombo vya habari viliripoti kuwa kuna mkazi mmoja Buruguni jijini Dar es Salaam alikuwa ameuganisha bomba lake la majitaka katika bomba la majisafi la DAWASCO. Habari hiyo ilishitua watu wengi sana kusikia kuwa kuna mwenzetu ambaye alikuwa ameamua sio kuhujumu tu mamlaka ya maji bali hata kuua wakazi wenzake kwa kuwanyesha kinyesi cha familia yake.

Haingii haraka akilini kuelewa mtu huyo alikuwa na lengo lipi kuchukua uamuzi huo. Nadhani vitendo kama hivi vinapaswa kudhibitiwa na kulaaniwa kwa vile ni kitendo ambacho sio tu harasa kwa DAWACO bali kinaweza kusaabisha kifo kwa mamia ya watu wanaoishi katika eneo hilo.

Tukio hilo limetuonyesha kuwa huenda sababu kubwa ya kipindupindu kuweka makazi yake maeneo ya buruguruni, vingunguti na ilala na Mwanyamala huenda wapo watu wengi wanaofanya hujuma kaa hizo katika miundombinu ya mamlaka ya maji.

DAWASCO kwa muda mrefu imekuwa ikilalamikia vitendo vya baadhi ya watu kuhujumu miundombinu yake kwa kuiba vifaa ya kuwezesha usambazaji wa maji na wengine kujiunganishia maji kienyeji ambayo wamekuwa wakiyatumia bila ya kulipia huduma hiyo.

Ni jambo la kushangaza kuwa sisi wananchi tunashiriki katika hujuma hizi za kujiuganishia maji kinyemela na kuiba vipuri vya kusaidia usambazaji wa maji, lakini ndio tumekuwa mbele kulalamika kuwa hatupati maji ya uhakika.

Tuelewe kuwa mamlaka za maji nchini zinajiendesha kwa kutumia mapato yanaypotokana na makusanyo ya ankara za huduma za maji, kama watanzania wengi tutatumia ujanja unjanja wa kupata maji bila ya kulipia na kuiba vipuri vya miundo mbinu, taasisi hizo zitajiendesha vipi?

Ni wazi kuwa utamanduni wa kuiba na kuharibu miundombinu ya miradi mbalimbali haitatufikisha mahali kokote watanzania . Sasa umefika wakati kwa kushirikiana na mamlaka hizo, vyombo vya dola watanzania wote kila mmoja awe mlinzi wa mali za umma ili akimwona mtu anayehujuma atoe taarifa polisi au ofisi za serikali.

Bila ya kuwa na uzalendo wa aina hiyo, miundomibinu yetu itaendelea kuhujumiwa na watu wachache kwa manufaa yao binafsi huku wakituacha tukiwa hatupati huduma.

Tukiacha hivi hivi, sio ajabu siku moja hata mtambo wa kusukuma maji wa Ruvu chini mkoani Pwani nao ukahujumiwa.

Hukumu iliyotolewa kwa wakazi wawili wa jijini kwenda jela kifungo cha miaka mitano kutokana na kuhujumu miumndombinu ya DAWASCO nadhani itatoa fundisho kuwa sasa ukichezea mali ya miradi ya maendeleo utakiona cha moto.

Haiwezekani katika nchi ambayo inafuata utawala wa sheria mtu ajiamulie kufanya analotaka hata kama litakuwa la kurudisha maendeleo nyuma, kuiba mita mabomba ya maji au nyaya za umeme ni uhuni ambao unapaswa kukemewa na wapenda maendeleo wote.

Watanzania ni watu ambao wanapenda sana maendeleo, lakini baadhi ya wanzetu bado na wakasumba za enzi ya ujamaa kuamini kuwa mali ya shirika la umma haina mwenyewe unaweza kujichukjulia tu.

Kasumba hii ndio ambayo kwa kiasi kikubwa ilifanya baadhi ya mashirika na makampuni ya umma ya umma tuliyokuwa tukiyaendesha kufa na mengine kujiendesha kwa hasara kutokana na watendaji wake na wananchi kujichukulia mali zake wakidai ni za umma.

Mwacheni Hamad apige kura


WIKI hii joto la Uchaguzi Mkuu wa rais na wabunge unaotarajiwa kufanyika Oktoba 30 mwaka huu nchini
lilimwuguza Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Seif Shariff Hamad ambaye katika hali isiyokuwa ya
kawaida alizuiwa kujiandikisha katika Daftari la Wapigakura visiwani Zanzibar kwa madai kuwa sio mkazi
wa eneo hilo.

Tukio hilo lilitokea katika Kituo cha uandikishaji cha Mtoni Kidatu kilichopo jirani na nyumbani kwa
Hamad baada ya Msimamizi wa kituo hicho Suleiman Ame kueleza kuwa kiongozi huyo wa Chama cha upinzani
hawezi kumwandikisha kwa sababu hana sifa ya ukaazi wa kawaida katika eneo hilo.

Msimamizi huyo alisema kuwa ili mtu aweze kuwa na sifa ya kuandikishwa katika daftari la wapiga kura ,
anatakiwa awe ameishi katika jimbo husika kwa muda wa miezi 36 mfululizo na kwamba kipengele hicho ndicho
kinachombana Hamad kuandikishwa.

Naye Sheha wa Shehia ya Mtoni Kidatu, Haji Abdulrahma alisema pamoja na kuwa anamtambua Hamad,
lakisi si mkazi wa eneo hilo kwa vile hajakaa hapo kwa
miezi 36 mfululizo.

Alisema mara nyingi amekuwa akimpelekea Maalm Seif barua mbalimbali za wito na nyingine za kumtaka
ashiriki katika shughuli za maendeleo za Shehia yake,lakini amekuwa haonekani na kwamba amekuwa haishi
katika nyumba yake.

Sheha huyo alikwenda mbali zaidi na kudia kuwa katika kuonyesha kuwa Hamad haishi katika eneo hilo hata
matangazo ya vifo ambayo amekuwa akitumiwa salama yamekuwa yakieleza kuwa habari hizi zimfikie mahali
kokote alipo.

Tukio hilo la kuzuiwa kujiandikisha kwa Maalim Seif ambaye pia ni Waziri Kiongozi Mstaafu linashangaza,
kwa sababu hakuna mtu asiyejua kuwa Hamad ni mkazi eneo hilo kwa nini leo anaonekana kuwa sio mkazi?

Mzengwe huo uliofanywa na msimamizi wa kituo cha uandikishaji wapigakura kumzuia Hamad kuajinadikisha
ni dhahiri ni chokochoko zinazofanywa kwa ajili ya kuzusha vurugu nyingine visiwani.

Ni juzi tu watu wartatu walijeruhiwa huku mmoja wao Khamis Juma Issa akielezwa kuwa katika hali mbaya
baada ya kuzuka vurugu katika kituo cha unadikishaji wapiga kura cha Kikuni Chemchem katika jimbo la Mwera,
Mkoa wa Mjini Magharibi.

Nasema ni tukio lilifanywa makusudi kwa ajili ya kuchochea ghasia kwa sababu maelezo yaliyotolewa na
Msimamizi kumzuia Hamad kuandikishwa hayana uzito wowote zaidi ya kujaa siasa zenye chuki.

Huwezi kusema kuwa Hamad sio mkazi wa eneo hilo eti kwa sababu amekuwa hashiriki katika shughuli za
maendeleo za eneo analokaa na kwamba amekuwa haonekani
mtaani.

Msimamizi wa Kituo cha Uandikishaji anapaswa kuelewa kuwa Hamad ingawa hayupo tena kwenye utumishi wa
serikali ni Katibu Mkuu wa chama cha siasa ambaye ana majukumu mbalimbali yanayomfanya asafiri mara kwa mara
badala ya kukaa barazani akicheza bao.

Hakuna kiongozi wa chama kikubwa cha siasa ambaye anaelewa majukumu yake anaweza kushinda barazini
akinywa kahawa na kula tende na harua kila siku labda atakuwa anaendesha familia na sio chama.

Hata ukiwa kiongozi wa familia huwezi kushinda kutwa nzima kila siku barazini ukipiga gumzo bila ya kutoka
kwenda kutafuta chochote, vinginevyo utakuwa unafanya biashara ya ajabu isiyoeleweka.

Hivyo, Suleiman na wenzake wanapaswa kuelewa kwa wadhifa wake Hamad lazima asafiri kwenda jijini Dar es
salaam na hata nje ya nchi kwa ajili ya kuhudhuria washa , mikutano ya kimataifa na shughuli nyungine.

Nafikiri Mheshimiwa Suleiman anataka kuifananisha kazi ya Usimamizi wa uchaguzi au usheha, na ukatibu Mkuu wa
chama, kitu ambacho hakifanani kabisa! Hata makatibu wengi wa vyama vya siasa hapa nchini kama vile Philip
Mangula (CCM), Polisya Mwaiseja (NCCR-Mageuzi), Dk. Wilbroad Slaa (CHADEMA) hawaonekana kila siku barazani
kwenye nyumba zao, wanashughuli nyingi mno zinazowafanya hata wasahau kula chakula.

Vile vile, kwa upande wa madai kuwa Hamad sio mkazi wa eneo hilo kwa sababu hata anapotumiwa salama za
vifo wanaomtumia wamekuwa wakieleza kuwa habari zimfikie mahali popote alipo, ni sababu za kitoto
ambazo zinaonyesha sasa siasa za Zanzibar zinakwenda upogo.

Kwani mtu kumtumia taarifa za msiba na kueleza kuwa habari zimfike mahali alipo ni kuwa hajulikani
anapoishi? Nadhani sasa umefika wakati ambao Wazanzibar mpaswa kukaa na kuelewa kuwa vurugu
zinazotokea zinasababishwa na nyinyi wenyewe.

Maalim Seif hata kama ana makosa yake basi anapswa kuadhibiwa kwa yale aliyotenda sio haya ya kuwekewa
mizengwe ya kujiandikisha wakati ukweli upo wazi kuwa
ni mkazi wa eneo hilo.

Kwa upande wake Hamad anapaswa naye kudhibiti baadhi ya wafuasi wake ambao wamekuwa wakidaiwa kufanya
chokochoko kadhaa katika maeneo ya kujiandikishia wapigakura ili kuepusha Zanzibar katika umwagaji wa
damu.

Wakati dunia imekodolea macho Uchaguzi wa rais na wabunge Zanzibar kutokana na historia ya nyuma , CUF
na CCM wanapswa sasa kuwatuliza wanachama wao kupunguza munkari ili uchaguzi ufanyike kwa njia ya
utulivu zaidi.

Hivi sasa dalili za kuzuka vurugu zimeanza kuonekana kutokana na matukio ya vurugu na watu kujeruhiwa
wakati huu wa kujiandikisha kupiga kura. Kama sasa watu wameanza kujeruhiana itakuwaje wakati wa uchaguzi
wenyewe nafikiri itakuwa kuchinjana. Hilo hatulitaki liotokee kabisaa!

Mipango hii ifanikiwa basi isiwe longolongo

WIKI hii serikali ilitamka bungeni kuwa inafanya jitihada za kushirikiana na kampuni moja ya China kuzalisha gesi iliyosindikwa ili iweze kutumika kama mafuta ya magari badala ya petroli na dizeli.

Uamuzi huo wa serikali unatokana na baadhi ya wawekezaji waliopatikana mwaka 2004 na mwaka jana wa kuzalisha gesi iliyosindikwa kuiwekea masharti mbalimbali serikali.

Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Lawrence Masha aliliambia bunge kuwa China imepiga hatua kubwa katika teknolojia hiyo na tayari ujumbe wa Shirika la Maendeleo la Petroli (TPDC) limeitembelea nchi hiyo Novemba mwaka jana.

Alisema nchi hiyo pia imekubali tena kugharimia ujumbe mwingine wa Mei mwaka huu wa kujifunza kuhusu teknolojia na sera za China zilizowezesha mafanikio makubwa katika utumiaji wa gesi asilia, sio tu kwenye magari lakini pia utumiaji wa gesi asilia kwa ajili ya kupikia majumbani na kwenye taasisi.

Kampuni ya awali iliyopatikana mwaka 2004 mwekezaji huyo aliweka sharti kwamba kampuni nyingine zisihusike katika usambazaji wa gesi hiyo badala yake yeye ndiye pekee aruhusiwe kufanya hivyo.

Kwa hakika habari hiyo ni njema, kwa sababu itatuwezesha watanzania kupata mafuta ya kuendeshea magari na mitambo kwa urahisi na kwa bei nafuu.

Nasema habari hii ni njema kwa sababu hakuna sababu yoyote ya sisi watanzania kupata tabu ya kununua mafuta kutoka urabuni wakati tuna nishati mbadala ya gesi ambayo inaweza kutumika kama mafuta.

Nadhani hata wazoi hili la kuanza kuitumia gesi tunayozalishaji kutoka Songosongo na Mnazi bay baadaye kwa ajili ya kuendeshea magari limechelewa kutolewa kutokana na ukweli kwamba nishati hii mbadala, tunaihitaji kwa udi na uvumba suku nyingi.

Kupanda kwa bei ya mafuta katika soko la dunia ni moja ya sababu kubwa ya kupanda kwa gharama za uzalishaji wa bidhaa nchini. watanzania hatuna haja ya kuathirika na bei ya mafuta katika soko la dunia wakati mwenyezi Mungu ametujalia kuwa na gesi asili ambayo tunaweza kuitumia kama mafuta.

Ni jambo la ajabu sana watanzania kulia kupanda kwa bei ya mafuta katika soko la dunia wakati, sisi tuna hazina kubwa ya nishati ambayo tayari tumeanza kuitumia.

Hii ni sawa na hadithi ya mabahari waliokuwa wakisafiri na meli katika mto mkubwa sana walioishiwa na maji ya kunywa wakaomba msaada wa kuletwa maji wakifikiria kuwa wapo katika bahari ya maji chumvi.

Waliopigia kuwaoamba msaada walichofanya ni kuwaambia washushe ndoo katika maji waliyokuwa wakisafiria kuchota maji.

Hata hivyo, pamoja na habari hiyo njema iliyotangazwa na serikali , lakini wasiwasi wetu watanzania ni kuwa , serikali imekuwa na kawaida ya kupanga mipango mingi ya maana lakini utekelezaji wake umekuwa ukibaki katika makablasha wizarani.

Pia mawaziri wengi wamekuwa hodari wa kueleza mipango mingi inayotekelezwa na serikali bungeni wanapojibu maswali ya wabunge lakini mipango hiyo huwa haitekelezeki.

Naamini waziri Masha alivyoeleza nia hiyo ya serikali haikuwa akitania ni mambo ambayo yapo katika mchakato wa kukamilishwa.

Kama alivyosema kuwa serikali imeshindwa kukubali zabuni ya mwekezaji mmoja ambaye aliiwekea sharti kupewa ukiritimba kusambaza kwa watumia yeye mwenyewe.

Masha alisema wizara yake inawasiliana na wizara ya fedha kuweka vivutio kwa wawekezaji na watumiaji hasa kutokanana gharama kubwa za usambazaji wa gesi asilia.

Alisema sera nzuri na vivutio vitaiwezesha serikali kuhimiza kwa ufanisi matumizi ya gesi asilia kwenye gari na kwa ajili ya kupikia na kuokoa fedha za kigeni kuagiza mafuta na kupunguza matumizi ya kuna na mkaa.

Tuaamini kuwa umakini huo utasaidia kupatikana mzabuni bora na kwa haraka ambaye atasaidia kuwaondolea kero watanzania.

Lakini wakati tukisubiri neema hiyo, serikali pia haina budi pia kubuni nishati nyingi mbadala za mafuta kama vile kuanzisha viwanda vikubwa kwa ajili ya kusindika mbegu za mti wa Jatropher ambao unatoa mafuta ya diseli na malighafi kwa ajili ya kutengenezea sabuni.

Mti huu unastawi kila mahali hapa nchini na kwamba una sifa moja kubwa kuwa unaweza kuvumilia unaweza kustawi hata katika sehemu ambazo ni kame.

Kuanzisha viwanda hivyo kutasaidia kuongeza uzalishaji wa mafuta ya diseli hapa nchini pamoja na kuongeza ajira kwa mamilioni ya watanzania.

Nasema itaongeza ajira kwa sababu asilimia 60 ya watanzania wanaishi vijijini ambako kilimo cha zao hili ndiko kitafanyika kwa wingi.

Majeraha jumuia tuliyopaya 1977, bado hayajatupa somo?

WIKI hii Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Diodorus Kamala,aliwawaambia watanzania kwamba tume maalum ya iliyoundwa na serikali kukusanya maoni kuhusu Jumuia ya Afrika mashariki inatarajiwa kuanza kazi Oktoba 13 mwaka huu.

Kamala aliwataka waananchi kujitokeza kutoa maoni yao kuhusu muundo wanaoutaka katika jumuia hiyo kabla ya kuanza rasimi kwa ushirikiano huo.

Aliwataka wadau wote wakiwamo viongozi wa vyama vya siasa, madhehebu ya dini, mashirika yasiyo ya serikali, dola, wanasiasa na watu mbalimbali kushiriki katika kutoa maoni yao.

Dhima kuu ya kuundwa kwake ni kukusanya maoni ya wananchi wa Tanzania yatakayotumiwa kuboresha muundo na kazi za jumuiya hiyo kuelekea kwenye shirikisho.

Kamati hiyo itafanya shughuli zake kwa kipindi cha miezi sita, na itatembelea makao makuu ya mikoa na wilaya zote nchini.

Kwa hakika sasa nafasi ambayo watanzania walikuwa wakiitaka ya kushirikishwa katika ushiriki wa nchi yao katika jumuia ya Afrika Mashariki imewadia.

Ni wazi kwamba Watanzania watakaojitokeza mbele ya kamati hiyo watatoa maoni yao kwa kuzingaitia historia ya Tanzania na maslahi ya wananchi wenzao ambao hawatapata nafasi kama hiyo.

Sio jambo la siri kwamba watanzania wengi mpaka sasa hawaelewi sababu za Tanzania kuingia katika ushirikiano wa Afrika Mashariki ambayo mwaka 1977 ilivunjika na kuwapa hasara kubwa.

Pia mpaka sasa hawaelewi faida ambayo watapata iwapo Tanzania itagingia katika shirikisho kamili na kama makosa yaliyosababisha kuvunjika kwa jumuia iliyopita yamesahihishwa na nchi jirani za Kenya na Uganda.

Kwanza kabisa napenda kuwaeleza watanzania wenzagu kuwa waitumie fursa tuliyokuwa tunaisubiri ya kueleza msimamo wetu kuhusu shirikisho hili na kwamba tutoe maoni yetu kwa uwazi bila ya kumwogopa mtu.

Tanzania ni nchi yetu, haituwezi kuigawa kama pipi kwa mtu mwingine, ni vyema tukaridhia wenyewe uamuzi wowote tukaouchukua bila ya shikinizo kutoka kwa nchi yoyote au kwa taasisi fulani.

Kwa bahati mbaya, Watanzania wengi hupenda kutoa maoni baada ya uamuzi kuwa umeshapitishwa, ni vyema kwa sasa tujenge tabia ya kupenda kujua mambo na kutoa maoni yetu kwa wakati mwafaka.

Ajenda ya shirikisho inatakiwa kujadili katika maeneo yote kuanzia shuleni, misikitini, makanisani na hata kwenye baa. Na hata mijadala mikali ianzishwe na wasomi katika vyuo vya elimu ya juu kujadili suala hili nyeti.

Kwa ujumla ni kwamba watanzania tunapaswa kutafakari kwa makini zaidi kuhusu suala hili la kuingia katika jumuia ya Afrika Mashariki kutokana na historia ya jumuia hii. Jumuia hii haikuzaliwa leo ilikuwapo huko nyuma lakini watatu chache wakaiwekea mkono mchafu mpaka ikavunjika.

Tukirejea nyuma, tujiulize nani aliyevunja Afrika ya Mashiriki iliyopita? Ni dhahiri sio watanzania ni bali wenzetu Wakenya na Waganda kutokana na sababu zao za kisiasa.

Watanzania wakati huo chini ya utawala wa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere walionekana kama vile walikuwa wasindikizaji katika jumuia hiyo ndio maana hata walipotaka kuivunja walifanya hivyo kwa manufaa yao.

Kama ambavyo nimekuwa nikihoji siku zote je ni sababu zipi zimewafanya leo Wakenya na Waganda kuutaka ushirikano huu wa Afrika mashariki kwa nguvu zote tena? Nadhani watanzania tunapaswa kutafakari kwa makini vinginevyo hawa wenzetu watatugeuza kuwa mbuzi wa shughuli.

Hivi sasa wananchi wa nchi hizi tatu, ni sawa tumelala kitanda kimoja lakini kila mmoja anaota ndoto yake kuhusu jinsi atakavyofaidika na ushirikano huu.

Kwa vyovyote vile Wakenya wanawaza na kutamani shirikisho litakapoanza watamaliza matatizo yao ya ardhi, ukosefu wa ajira kupitia Tanzania na Uganda, Waganda hususan kiongozi wao Yoweri Museven wanapenda sana sifa, wao ndoto yao kubwa wanaota kuitawala Afrika Mashariki Mashariki.

Swali ambalo watanzania tunatakiwa kujiuliza ni kwamba wakati wenzetu wanawaza hayo, sisi Watanzania ajenda yetu inayotusukuma kuingia katika shirikisho hilo ni ipi? Ni kuwekeza katika nchi hizo? , sifa ya kuwa Afrika Mashariki tumeungana au ni ushabiki tu wa ngoma inayopita mtaani kwetu ambayo hatuijui madhumuni yake?

Kitu kingine ambacho watanzania tunapaswa kukijadili wanakati tunapotoa maoni yetu kuhusu shirikisho la Afrika Mashariki ni kuingia kwa nchi za Rwanda na Burundi katika Jumuia hiyo.

Wenzetu hawa wanajulikana bayana kutokana na nchi zao kukosa utulivu unaosabishwa na migogoro isiyoisha na ndani za nchi zao inayosababishwa na ukabila na uroho wa madaraka.

Baadhi ya watu wameaanza kuwa na wasiwasi kama ni vyema kuwa na watu kama hawa katika jumuia yetu. Ingawa wapo wanaosema kuwa huenda nchi hizo zikaiga ustarabu wa watanzania zikiwa ndani ya jumuia.

Kutokana na hali hiyo, tume maalum iliyoteuliwa kufanya kazi ya kukusanya maoni kuhusu Jumuia ya Afrika Mashariki nayo inapaswa kuwa makini ili isije ikatoa ripoti ambayo nyuma yake inashinikizo la mtu au nchi fulani.

Tunajua kuwa hivi sasa baadhi ya wananchi wa Kenya na Uganda wameanza kueleza kuwa Tanzania inasita kuingia katika jumuia kutokana na hofu ya ardhi kuchukuliwa na wageni. Kutokana na wenzetu hawa kujua hofu yetu wasije wakaitumia katika kushikiza ili mambo yao yaende wanavyotaka.

Bajeti ya mwaka huu iboreshe maisha ya watanzania

WAZIRI wa Fedha, Zakia Meghji wiki hii alitoa sura ya bajeti ya serikali ya mwaka ujao ikionyesha kuwa jumla ya Sh4.8 trilioni zitatumika katika kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.

Waziri alieleza kuwa bajeti ya mwaka ujoa imejengwa katika misingi ya ilani ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2005 na kwamba fedha zitapelekwa katika maeneo ambayo muhimu kwa ajili ya kuboresha maisha ya watanzania.

Kati ya fedha hizo, kiasi kikubwa kikiwa kimeelekezwa kwa Wizara za Elimu na Mafunzo ya Ufundi, kilimo, Elimu ya Juu, Sayansi na Teknolojia, Usalama wa Raia, Afya na Ustawi wa Jamii na Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.

Katika bajeti hiyo, Sh3.1 trioni zimetengwa kwa matumizi ya kawada wakati 1.7 trilioni miradi ya maendeleo. Katika bajeti hiyo ambayo itatangazwa Juni 15, Sekta ya Kilimo imepewa kipaumbele zaidi kwa kupatiwa jumla ya sh bilioni 333.

Katika bajeti ya mwaka 2005/2006 serikali ilitenga kutuymia sh trioni 4.17. Kwa maana hiyo kuna ongezeko kidogo katika bajeti ya mwaka huu.

Sio nia yangu kuanza kuchambua takwimu zote zilizopo katika sura hiyo ya bajeti bali ninataka kuwapa wasomaji wangu angalu kwa muhtasari bajeti hii ilivyo.

Baadhi ya shughuli muhimu ambazo zimepatiwa mgawo zaidi wa fedha kwa kuzingatia ilani ya uchaguzi wa CCM ni hifadhi ya mazingira iliyopata sh bilioni 9.4, ruzuku 21 badala ya sh bilioni saba mwaka jana.

Pia bajeti ya mwaka ujao kwa mujibu wa Meghji serikali imetenga kwa ajili ya kuwapandishia mishahara watumishi wake.

Ingawa serikali inalenga kukusanya mapato ya ndani yasiyopungua Sh trilioni2.5 trilioni ikilinganishwa na mapato ya Sh2.06 ya mwaka 2005/06. Ongezeko hilo litakuwa ni asilimia 19.1.

Kwa hakika kuongezwa kwa bajeti ya kilimo kutasaidia kuwapatia ajira watu wengi zaidi vijijini.

Hata hivyo, ingawa serikali imeongeza fungu katika kilimo kama hakutakuwa na mikakati mizuri ya namna ya kuwapunguzia umasikini wananchi kwa kutumia rasmali zetu hazitasaidia kitu.

Kwa mfano hivi sasa mabebki mengi nchini hayawezi kutoa mikopo kwa wakulima wadogo kutokana na kuwa na sera ambazo zinahitaji mtu kuwa na dhamana kubwa.

Je mkulima wa jembe la mkono aliyeko mbinga ataweza kukwamua vipi na umasikini kama hataweza kuwa na uwezo wa kwenda kukopa benki kupata mtaji utakaomwezesha kupanua kilimo chake?

Kwa upande wa hela azilizotengwa kwa ajili ya ruzuku ya mbolea, bado nako kwa upande hakuna usimamizi mzuri wa usamabaji wa mbolea hii.

Tunaendelea kushuhudia mbolea ya ruzuku kwa wakulima wa mikoa ya nyanda za juu kusini wanalia kuwa wanauziuwa mbolea hiyo na wafanyabiashara kwa bei ya juu ambayo hiana punguzo.

Kwa upande wa ogezeko la la mapato ya ndani, ingawa serikali imesema kuwa katika bajeti ijayo inatarajia kuongeza mapato ya ndani ya kwa asilimia 19.1 kutoka sh trioni 2.06 hadi sh trioni 2.4, misamaha ya kodi inayotolewa na serikali kwa waagizaji wa bidhaa kutoka nje inapunguza mapato haya.

Hivi sasa taarifa zilizopo zionanyesha kuwa karibu asilimia 30 hadi 40 ya makusanyo ya ndani kwa mwezi hurudishwa kwa walipokodi kama misamaha ya kodi.

Nadhani kuna umuhimu sasa sheria ya misamaha ya kodi ikarekebishwa ili baadhi ya watu au taasisi zikaondolewa katika misamaha ya kodi.

Hivi sasa watu wengi wanatumia mwanya huo, wa kuwapo kwa mlolongo wa makundi mengi yanayoruhusiwa kupewa misamaha ya ushuru wa forodha kukwepa kulipa ushuru na hivyo kuikosesha mapato serikali.

Suala jingine ambalo nadhani ni muhiumu katika bajeti hii likaangaliwa kwa umakini ni ubadhilifu wa fedha za mabilioni katika halmashasuri.

Ingawa serikali imeeleza katika bajeti ya mwaka ujao itaajiri wahasibu wawili kwa kila halmashauri ili kuongeza udhibiti wa fedha kupotea, lakini watumishi hao nao hawaagaliwa kwa karibu nao watataweza kuzitafutana fedha hizi za walipa kodi.

Tatizop la ulaji wa fedha katika halmashauri ni kubwa na kwamba baadhi ya mawadiwani kwa kushirikiana na wakurugenzi wa halamshauri hushirikiana kuweka matumizi hewa na fedha hizo kuingia mifukoni mwao.

Ni vyema sasa serikali ikawaeka utaratibu unaowabana watendaji wa halamshauri kutafuna fedha.

Suala jingine ambalo katika bajeti hii tunaomba lifanyiwe kazi ni
Kwa vitambulisho vya urai. Sisi wananchi tunashindwa kuelewa nini kinachokwamnisha suala hili licha ya serikali kueleza kila mara kuwa inaendelea na mchakato wa utekelezaji.

Hivi sisi ni vipofu katika uigiaji wa mikataba ya kuuza mali zetu?

WIKI hii watanzania walipata faraja baada ya kusikia kwamba serikali imelirejesha Shirika la Ndege Tanzania (ATC) mikononi mwake baada ya Shirika la Ndege la Afrika Kusini (SAA) kukubali kuiuzia hisa ilizokuwa ikizimiliki kwa bei ya dola moja ya Marekani.

Mwenyekiti wa Bodi ya ATCL, Ali Mufuruki alisema kuwa SAA imekubali kurejesha hisa zake asilimia 49 ilizozinunua mwaka 2002 baada ya mazungumzo ya ujumbe wa Tanzania na serikali ya Afrika Kusini yaliyofanyika Agosti 29 Agosti mwaka huu.

Alisema sababu kubwa iliyofanya serikali kulirejesha shirika hilo katika umiliki wake ni kupishana kwa mipango ya kibaishara baina ya wabia wa kampuni.

Mwenyekiti huyo wa Bodi alisema baada kurudishwa katika umiliki wa serikali, ATCL imebuni mkakati wa kununua ndege nne zaidi ili kulifanya shirika hilo kufikisha ndege sita hadi katikati ya mwaka ujao.

Akizungumzia hali ya kifedha ya shirika hilo, alisema linapata hasara ya Sh1 bilioni kwa mwezi hali inayoifanya serikali iendelee kulipa ruzuku ya uendeshaji.

ATCL ambayo inabakia katika mwenendo wa ubinafishaji chini ya Tume ya Rais ya Kurekebisha Mashirika ya Umma (PSRC) baada ya ndoa yake na SAA kuvunjika rasmi Agosti 29, mwaka huu, inatakiwa kujiimarisha kifedha ndani ya miaka miwili ili liweze kupata mbia mwingine kwa bei ya kuridhisha.

Kwa hakika kuvunjika kwa mkabata huu wa ATCL na SAA ni fundisho tosha kwamba mikataba mingi ambayo tumeingia katika kuyauza mshirika yetu haikuwa na maslahi kwa taifa bali ilikuwa ni kwa ajili ya watu wachache tu.

Nasema hivyo kwa sababu tumeshuhudia mikataba mingi ya uuzaji wa masharika yetu ambayo sasa imegeuka kuwa shubiri kutokana na watanzania wezetu ambao tumewapa dhamana ya kuuza mashirika yetu ama kuangalia zaidi maslahi yao binafsi.

Nakumbuka ATC ilipouzwa kwa SAA kila mtu alishangilia sana kwamba sasa shirika letu la ndege ambalo lilikuwa linachechemea sasa litakuwa shirika kubwa la ndege katika Afrika lenye ndege za kileo na wafanyakazi ambao wana viwango vya kimataifa.

SAA katika moja ya ahadi zake iliteua mji wa Dar es Salaam kama kitovu chake cha biashara katika nchi za Afrika Mashariki kama njia ya kuwa baadaye kiungo muhimu cha biashara kati yake na nchi za mashariki na magharibi za Afrika.

Shangwe hizo za watanzania hazikuendelea kwa muda mrefu baada ya ATCL kuanza kukumbwa na wingu la mvutano kati ya Tanzania na SAA baada ya kushindwa kutekelezwa kwa ahadi kadhaa zilizotolewa na mwekezaji.

Mlalamiko ya kwanza ya Tanzania yalikuwa kutokutekelezwa kwa makubaliano ya awali kati yake na SAA, likiwemo suala la kushindwa kuimarisha ATCL kwa kuongeza njia zake katika sehemu mbalimbali duniani kama ilivyokuwa imekubaliwa.

Mengine yalikuwa ni kwamba, SAA ilikuwa inakodisha ndege zake kwa ATCL kwa gharama kubwa kuliko bei halisi na kwamba mifumo ya tiketi, malipo na namba za ndege ilikuwa inawategemea SAA.

Kutokana na malalamiko hayo, Tanzania iliamini kuwa Afrika Kusini wanakusudia kuiua ATCL ili kupunguza ushindaji katika biashara ya usafirishaji kwa njia ya anga.

Mbali ya kushindwa kutimiza ahadi za SAA ilikuwa ikikaidi ushauri wa serikali ya Tanzania katika mambo kadhaa ambayo ilitaka yatekelezwe kwa mujibu wa mkataba.

Kutokana na mbia huyo kukaidi ushauri na kulalamika mara kwa mara kuwa amekuwa akipata hasara ili kuhakikisha shirika hilo linaendelea kuwepo hadi litakaporejea mikononi mwake, tangu mwishoni mwa mwaka jana ilianza kutoa Sh500 milioni kila mwezi.

Kimsingi, Sipingi mkakati wa serikali wa kujenga uchumi wa soko. Na pia ninaamini kuwa si kazi ya serikali kutengeneza na kuuza vibiriti na vijiti vya kuchokonolea meno lazima kazi nyingine zitafanywa na watu binafsi.

Nikirejea katika hoja yangu ni wazi kwamba ubinafsishaji wa mshirika yetu hakuna mtu anayeupinga,ila kinachopingwa hapa ni namna zoezi hilo linavyoendeshwa.

Mashirika ya umma yameuzwa kwa bei ya kutupa na kwamba hata mikataba yenyewe imekuwa kama vile ni bangi au dawa za kulevya ambayo haitakiwi kuonwa na mtu au umma kuelewa kinachoendelea.

Usiri huu ndio ambao umetufikisha katika hali hii ya mashirika yetu yakiwa katika hali nzuri lakini yanapouzwa au kukodishwa tunarejeshewa yakiwa katika hali mbaya.

Hali hiyo inatoa sura kwamba huenda rushwa katika zoezi hilo imeghubika ndio maana wapo watu ambao ni watanzania wenzetu wanatoa mashirika haya kwa watu kwa bei ya njugu huku wakielewa kuwa ni kuwafikisha watanzania katika hali mbaya.

Tunashukuru hatua ya serikali kuipitia upya mikataba ya madini ambayo imesaidia walau sasa watanzania tutapata hela kisia ingawa ukweli unabaki pale pale kuwa pamoja na kuwa madini mengi tunachopata hakiligani kabisa na utajiri huu.

Ni vyema sasa serikali ya awamu ya nne, ikajipanga upya hasa katika mikataba ya uuzaji wa mashirika au uwekezaji ili watanzania wafaidike na maliasili zao au makampuni yetu.

Pia mikataba ya uwekezaji au ununuzi wa mashirika ipitishwe na chombo kingine badala ya utaratibu wa sasa wa kupitishwa na baraza la mawaziri ambalo mwenyekiti wake anakuwa ni rais.

Kama mkataba utakuwa mbovu hauna maslahi ya watanzania ni vigumu kwa rais kuwajibishwa watalaam waliohusika katika kushauri kwa sababu hata yeye aliupitisha katika ngazi ya baraza la mawaziri.

Viongozi wa serikali wanaohusika na uuingiaji wa mikataba, sasa lazima wabadilike, wawatumikie watanzania kwa kuingia mikataba ambayo ina maslahi ya nchi. Kama watu hawa watabadilika basi yaliyotokea kwa ATC, na DAWASA yataendelea kutokea.

Polisi sasa mnaelekea kubaya!

RIPOTI ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora kuhusu unyama unaofanywa na Polisi dhidi ya raia, umekiweka wazi kilio cha muda mrefu cha wananchi.

Ripoti hiyo ambayo iliyotolewa wiki hii na Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Robert Kisanga kwa waandishi wa habari inaeleza kwa undani jinsi polisi wanavyoshirikiana na majambazi kuwapora raia mali zao.

Jaji Kisanga katika ripoti hiyo ameeleza kuwa polisi wamekuwa wakitoa taarifa muhimu kwa majambazi zinazoyawezesha kuvamia raia na kupora.

Vile vile, alisema vituo vya polisi vimegeuzwa kuwa jehanamu kwa watuhumiwa kupigwa, kunyanyaswa na hata kulazimishwa kukiri makosa kutokana na kipigo wanachopata kutoka kwa polisi.

Kingine ambacho Kisanga alisema Tume yake imegundua ni kuwa vituo vingi vya polisi havina mahabusu na kwamba watuhumiwa wanawake wamekuwa wakilala kaunta pamoja na askari hali ambayo inasababisha kubakwa.

Tume hiyo imegundua pia kuwa hata katika vituo vichache ambavyo vina vyumba vya mahabusu, watuhumiwa watoto wamekuwa wakichaganywa na wakubwa hali ambayo inawafanya wapate manyanyaso na pengine kufanyiwa mambo mabaya na watuhumiwa wakubwa.

Kwa ujumla ripoti hii ya kwanza kufanywa na Tume hiyo, imesaidia kuanika hadharani maovu ambayo yanafanywa na baadhi ya askari wa Jeshi la Polisi dhihi ya raia.

Kwa muda mrefu wananchi wamekuwa wakilinyoshea kidole Jeshi la Polisi kuwa baadhi ya askari wake, wamegeuka kuwa majambazi na kwamba hata baadhi ya vituo vya polisi vimegeuzwa kuwa ni vituo vya biashara ambako haki yako lazima uinunue.

Kilichogunduliwa na Tume ya Jaji Kisanga kuwa askari wanashirikiana na majambazi ni kweli kwa sababu hakuna mtu asiyefahamu kuwa majambazi yote nchini yanafanya uhalifu kwa ushirikiano kutoka kwa baadhi ya askari polisi.

Ukitaka kujua kuwa baadhi ya askari wanashirikiana na vikundi vya ujambazi ni majambazi yanapovamia mahali hata kama wapaita tukio linatendeka hurudi baada ya saa au mbili wakati ambapo wahalifu huwa wameshaondoka.

Hakuna asiyejua jinsi majambazi yanayoazimwa  silaha na baadhi ya askari wa Jeshi la Polisi kwenda kufayia uhalifu kwa makubaliano ya malipo.

Kutokana na kuwepo ushirikiano mkubwa wa askari na majambazi imefikia mahali jambazi hivi sasa linaweza kukupa taarifa kuwa usiku wanakuja na wenzake kuchukua gari yako, ukitoa taarifa polisi huwa hakuna juhudi zozote zinazochukuliwa kukulinda

Jambazi hivi sasa likikamatwa likifikishwa polisi  baada ya siku mbili utaliona mitaani likiendelea kufanya uhalifu.
Kwa kweli hali ni mbaya askari polisi ambao jukumu lao ni kulinda raia na mali zao , hivi sasa wamebadilika kuwa askari ambao wapo kwa ajili ya kupora mali za wananchi na maisha yao.

Nani asiyeelewa kuwa hivi sasa ukiwa na mtuhumiwa wako unataka akamatwe ukienda polisi kutoa taarifa lazima utoe hela kwa ajili ya mafuta ya gari la doria usiku.

Haya ni mambo ya ajabu sana, wakati serikali ya Rais Benjamin Mkapa ikijitiahidi kuimarisha utalawa wa sheria, baadhi ya askari katika Jesi la Polisi wamekuwa kikwazo kikubwa cha juhudi hizo.

Kuhusu watuhumiwa wanawake, baadhi ya vituo vya polisi hivi sasa vimegeuka kuwa kichaka cha ubakaji  

Kutokana na vituo vingi vya polisi kukosa vyumba vya mahabusu, watuhumiwa wanawake wamekuwa wakiwekwa kaunta wanapokaa polisi na hivyo wengi kujikuta wakibakwa usiku na baadhi ya askari hao.

Wanawake wanaobakwa wakiwa polisi hushindwa kupeleka malalamiko yao kutokana na kupigwa mkawara mzito na pengine kubambikiwa kesi nyingine za bangi au dawa za kulevya wanapoonekana kutaka kudai haki zao.

Wananchi hivi sasa hawana imani tena Jeshi la Polisi kutokana na vitendo vya baadhi ya askari, hivyo wanapomkamata mhalifu wengi wanafikia uamuzi wa kujichukulia sheria mikononi kwa kuamini kuwa wakimpeleka polisi lazima ataachiwa.
Ili jeshi hilo liweze kurejesha heshima yake kwa raia, linapasa kuwaondoa askari wote wanaofanyakazi kinyume cha sheria zinazoliongoza jeshi hilo.

Bila kufanya operesheni ya kilisafisha , juhudi za serikali kutaka kuimarisha utawala bora na kuondoa rushwa hazitaweza kufanikiwa.
Askari polisi wanapaswa kubaki kuwa walinzi wa raia na mali zao na sio kuwa waporaji wa mali na maisha ya raia.

 

 

Kwa mwenendo huu, heshima yetu itarudi

SERIKALI imeanza kukagua majengo ya maghorofa yaliyojengwa katika maeneo mbalimbali nchi nzima, kwa kuanzia, tunaambiwa kuwa majengo zaidi ya 500 yatakaguliwa katika wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam.

Ukaguzi huu wa majengo unafanywa na timu maalum iliyoundwa kwa agizo la Waziri Mkuu, Edward Lowassa. Timu hiyo inaundwa na maafisa wa serikali kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na ile ya Miundombinu na itafanya ukaguzi huo katika kata zote za Manispaa ya Ilala zenye majengo ya maghorofa.

Siyo siri kwamba wilaya ya Ilala ndiyo inayoongoza kwa kuwa na majengo mengi na marefu zaidi ya ghorofa kwa nchi nzima. Eneo lote la Kariakoo na katikati ya jiji, ambalo ndilo eneo nyeti kibiashara lipo chini ya mamlaka ya manispaa hiyo.

Kuundwa kwa kamati hiyo, kunatokana na agizo la Lowassa, siku chache baada ya jengo la ghorofa la hoteli ya Chang'ombe Village Inn lililokuwa likijengwa, kuporomoka Machi 17, 2006 na kusababisha kifo cha mtu mmoja. Huenda wapo pia waliojeruhiwa au kupotea!

Jengo hilo liliundiwa tume na juzi ilikabidhi ripoti yake kwa Waziri wa Miundombinu, Basil Mramba, ikibainisha kwamba ujenzi mzima haukuzingatia sheria, taratibu na kanuni zinazokubalika.

Kosa jingine, ripoti hiyo imebaini ni la kiufundi ambalo ni pamoja na jengo hilo kukosa ramani ambayo ilipaswa kuthibitishwa na mamlaka husika au bodi ya ukadiriaji na usanifu majengo na kwamba hata kiwanja lilipojengwa hakikupimwa.

Kwa hakika, uamuzi huu wa kukagua majengo yote ya maghorofa ni muafaka ili kuyabaini ambayo hayakujengwa kwa kufuata taratibu.

Tukio la jengo la Chang'ombe Village Inn ` kuporomoka na kusababisha maafa limetuachia funzo kwamba huenda majengo kama hayo yapo mengi hapa nchini.

Wapo baadhi ya watu hapa nchini kutokana na uroho wa kupata fedha wamekuwa wakijenga majengo ya ghorofa bila ya kufuata taratibu ikiwamo kutokuwa na kibali halali cha ujenzi, kutumia wakandarasi feki.

Baadhi yao, tunasikia kwamba wanatumia hata vifaa duni ambavyo haviendani na taratibu za ujenzi wa nyumba, hususan maghorofa.

Kwa ujumla, nyumba zilizojengwa kwa mtindo huo ambazo naamini nyingi hapa nchini ni bomu ambalo likilipuka litaleta madhara makubwa kwa wananchi.

Lakini, ni nini kilichotufikisha hapa? Rushwa ni sababu kubwa kuliko sababu yoyote. Baadhi ya maafisa wa ardhi wengi kwa muda mrefu wamekuwa wakigawa viwanja kwa ajili ya ujenzi mijini kama njugu bila ya kuangalia ramani za mijini na taratibu nyingine zinazoongoza ujenzi.

Watu hawa wamekuwa wakijipatia fedha nyingi za hongo kutoka kwa matajiri hao wanaopindisha sheria ambao ndio wameingiza nchi katika migogoro mikubwa ya ardhi inayoendelea kufukuta nchini.

Hivyo, naamini kuwa hatua hii ya sasa ya serikali kuanza kukagua majengo itafichua mengi na ndiyo njia pekee ya kunusuru maisha ya Watanzania wengi ambao baadaye wangeangukiwa na majengo hayo.

Ni kutokana na ugawaji mbaya wa viwanja unaofanywa na baadhi ya maafisa wa ardhi ndio ambao umeifanya serikali katika Manispaa ya Kinondoni kuchukua uamuzi wa 'kubomoa' majengo mawili ya ghorofa nane kila mmoja yaliyopo eneo la bahari ya Hindi la Masaki jijini Dar es Salaam. Majengo hayo yanadaiwa kujengwa bila ya kufuata taratibu.

Watanzania, lazima tukubali hatuwezi kupata maendeleo kama kila mmoja ataamua kujifanyia jambo lake bila ya kufuata taratibu. Huwezi kuamua leo ukajenga nyumba mahali kokote hata kama haparuhusiwi kwa sababu tu una hela!

Kama hali hii itaachiwa iendelee sio ajabu siku moja tukiamka asubuhi na kukuta katikati ya barabara ya Mandela au Morogoro linajengwa ghorofa ambalo ni mali ya mwekezaji.

Hatua hii ya serikali ya awamu ya nne kuamua kuanza kukagua ujenzi wa majengo naamini utasaidia kuyaondoa majengo ambayo yamejengwa kinyume cha sheria na kuiweka miji yetu katika hali inayotakiwa.

Vile vile, hatua hii ya serikali itawaondolea kiburi matajiri ambao wanatumia fedha zao kupindisha sheria na kujifanyia mambo wanavyotaka. Kwa hakika, heshima itarejea kila mtu ataheshimu mamlaka zinazohusika.

Miji yote mikubwa duniani inaonekana mizuri ikiwa katika mpangilio ikipambwa na majengo marefu ya ghorofa, lakini haikujengwa holela kama ilivyo hapa kwetu, ramani ya mipango miji ilifuatwa pamoja na taratibu nyingine za ujenzi.

Wapo baadhi ya watu hivi sasa hapa kwetu bila ya kujali ramani ya mji wanajenga juu ya mabomba maji ya kunywa, maji machafu na kadhalika na wengine wanavamia viwanja vya wazi na wengine wanajenga hata chini ya nyaya za umeme wenye msongo mkubwa kana kwamba hawajui athari zake. Naamini, sasa watakuwa wameanza kupata somo.

Mwema sasa safisha polisi

RAIS Jakaya Kikwete wiki hii alifanya mabadiliko katika jeshi la polisi kwa kumteua, Said Mwema kuwa Inspekta Jenerali mpya wa polisi kuchukua nafasi ya Omar Mahita ambaye utumishi wake unakoma mwishoni mwa wiki hii.

Pia Rais Kikwete alimteua Robert Manumba kuwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai kushika nafasi iliyokuwa ikishikiliwa na Rajabu Adad ambaye ameelezwa kuwa atapangiwa kazi nyingine.

Mabalidiko mengine ambayo rais Kikwete aliyafanya katika jeshi la polisi ni pamoja na kumpandisha cheo kuwa Kamishna wa Polisi na kumteua Clowding Mathew Mtweve kuwa Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa Jeshi la Polisi, akijaza nafasi inayoachwa wazi na Kamishna Wilson Mwansasu ambaye anastaafu kwa mujibu wa sheria.

Mwingine aliyeteuliwa kuiongoza Idara ya Mafunzo na Operesheni ni Paul Amani Moses Chagonja, aliyepandishwa cheo kutoka Kamishna Msaidizi wa Polisi hadi kuwa Kamishna wa Polisi.

Rais Kikwete pia alifanya mabadiliko ya hadi ya utawala wa kipolisi katika Mkoa wa Dar es Salaam ambao sasa utakuwa ukijulikana kama Kanda Maalum ya Dar es Salaam, huku wilaya zake tatu zikipewa hadhi ya mikoa.

Alimpandisha cheo kuwa Kamishna, Alfred Tibaigana na kumteua kuwa Kamanda wa Polisi wa Kanda hiyo, akiwasimamia makamanda watatu wa polisi wa Temeke, Ilala na Kinondoni.

Kwa hakika mabadiliko katika jeshi la polisi yaliyofanywa na rais Kikwete yanakuja wakati watanzania walikuwa wakiyasubiri kwa hamu kubwa kutokana na kuongezeka kwa uhalifu ambao umekuwa ukihusishwa na askari wenyewe.

Ninampongeza Rais Kikwete kwa kufanya mabadiliko katika jeshi hilo na ninaamini kuwa mabadiliko hayo yasiishie hapo tu katika kulisafisha jeshi la polisi bali yaende kila mahali.

Sina mashaka na utendaji wa kazi wa Mwema, ambaye amekulia ndani ya jeshi la polisi hapa nchini kabla ya kuteuliwa kuwa Mkuu wa Ofisi ya Shirikisho la Polisi Duniani (Interpol) jijini Nairobi.

Ninaamini kuwa Mwema atatumia uzoefu alioupata katika kushika nyadhifa mbalimbali ndani ya jeshi la polisi pamoja na interpol kuhakikisha kuwa anamaliza uhalifu nchini.

Hata hivyo, kitu kikubwa ambacho anatakiwa kukifanya kwanza ni kulisafisha jeshi hilo kuanzia ngazi za chini hadi ya juu.

Sio siri kuwa bado kuna maafisa wa juu ndani ya jeshi hilo ambao ni wachafu wanaonuka rushwa, wanaonuka halufu ya dawa za kulevya na bangi.

Ingawa yeye ni wenzake waliochaguliwa na rias kushika nyadhifa hizo ni wasafi lakini kama ataewndelea kukaa na maafisa wachafu nao watamchafua na hatimaye kurudi kule kule tulikokuwa.

Ili aweze kuweka mambo sawa anapaswa sasa kupangua safu ya makamanda wa polisi wa mikoa ambao wengi wao waaminika kuwa ndio kiini cha kuongezeka kwa uhalifu katika maeneo yao.

Baadhi ya makamanda hao tayari majina yao yameshafikishwa kwa rais yakiwa yameambatana na tuhuma zao kuhusu kujihusisha na uhalifu au kuwasaidai wahalifu kufanya shughuli zao.

Mwema tuaamini kuwa wewe ni mtanzania ambaye umekaa na jeshi hili kwa muda mrefu unajua udhaifu uliopo hivyo haitakuchukua muda mrefu kuleta mabadiliko ya kweli ndani ya jeshi la polisi ili liweze kufanya kazi zake ya kulinda raia na mali zao.

Hivi sasa wananchi wamepoteza imani na jeshi la polisi kutokana na baadhi ya askari kujiingiza katika uhalifu na wengine kuwabambikia makosa wananchi ili waweze kujipatia.

Wapo askari wamefikia mahali pa kugeuka kuwa vibaka ambao wanapokutana na raia usiku mitaani wakiwa katika doria badala ya kuwapa ulinzi wanawapora vitu walivyonavyo.

Hatua hii imelipaka matope jeshi la polisi kiasi cha kuliacha uchi. Tunadhani kuwa sasa umefika wakati ambao Jeshi la polisi likiwa chini ya Mwema liwe safi ili wananchi wanaweze kurudisha imani.

Museven toto tundu linaloota usultani

MACHO na masikio ya watanzania kwa karibu siku 20 yalikuwa katika visiwa vya Zanzibar ambako uchaguzi mkuu wa rais na madiwani ulifanyika.

Uchaguzi huo ambao ulimazika Oktoba 30, 2005 kwa Mgombea urais kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Aman Karume kuibuka mshindi baada ya kumshinda mgombea wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad.

Hata hivyo, uchaguzi huo ulikumbwa na misukosuko kadhaa ikiwamo CUF kukataa matokeo kwa madai kuwa hakufanyika katika mazingira yaliyohuru na haki na baadhi ya nchi za magharibi kama Marekani na Norway kuelezea kuwa hakuwa huru na haki.

Wakati watanzania tunatathimini hali ya tete za kisiasa Zanzibar, habari nyingine za kushangaza tulizipata kutoka kwa ndugu zetu waganda kuwa Rais Yoweri Museven amechaguliwa na chama chake cha NRM kuwa mgombea urais.

Habari hizo zinashangaza kwa sababu, Museven ameanza harakati za kupata nafasi hiyo kwa muda mrefu, ingawa amekuwa akitaka umma uelewe kuwa wanganda ndio wanaomtaka aendelee kuwaongoza.

Harakati za Museven kuwania nafasi hiyo, zilianza baada ya kuibadili katiba ya nchi hiyo ili kumruhusu aweze kuwania nafasi ya urais kwa kipindi cha tatu.

Uamuzi huo wa Museven ulipigiwa kelele sana na baadhi ya waganda wapenda demokrasia na jumuia ya kimataifa, lakini aliziba masikio yake na nta na kupuuza yote aliyoshauriwa.

Baada ya watu kupiga kelele na kuonekana kuwa Museven ameziba masikio yake, waliamua kutulia na kumwachia aendelee na safari yake ya kuelekea kwenye udikteta.

Tukio la hivi karibuni la Mwanasiasa maarufu nchini humo, Dk. Kizza Besigye kurejea Uganda limezidi kummwonyesha Museven sura yake halisi tofauti na tunayemjua kijana wa Mwalimu Julius Nyerere ambaye amedumu katika utawala wa nchi kwa takribani miaka 20.

Serikali ya Museven wiki hii iliagiza kukamatwa kwa mpinzani wake wa kisiasa Dk. Besigye kwa madai ya kutaka kupindua serikali akishirikiana na wenzake 14 na kumbaka msichana na kumwambukiza ugonjwa wa ukimwi.

Kitendo hicho kimelaaniwa na waganda na jumuia ya kimataifa kwani ni dhahiri kuwa kesi hiyo dhidi ya Dk. Besigye ya kisiasa zaidi kutokana na nia yake ya kutaka kugombea urais kupitia kambi ya upinzani.

Tayari Dk. Besigye ambaye hapo awali alikuwa swahiba mkubwa wa Museven amefikishwa mahakamani kujibu mashataka ya kubaka na uhaini.

Kwa hakika kama nilivyowahi kumzungumzia Museven katika safu hii, ameonyesha dhahiri kuwa demokarsia kwake ni ndoto ya mchana.

Kudhihirisha kuwa Museven ni mtu ambaye hataki demokarsia na anataka kuufanya urais wa uganda kuwa ni usultani katika muda wote aliokaa madarakani, ameshindwa katika utawala wake hata kuruhusu kuwapo kwa vyama vingi zaidi ya kuruhusu vikundi vya vugungungu la kisiasa.

Mipango ya Museven anayoendelea nayo kuwaziba midomo wapinzania wake inatisha na kwamba watanzania sasa umefika wakati kumtenga hata kama ni mtoto wetu.

Ingawa Museven amelelewa na watanzania wakati akiendesha vita vya msituni vya kuiangusha serikali ya Unganda, lakini kwa vile ameota mapembe yanayomfanya aamue kuongoza nchi kwa mikono ya chuma, watanzania hatuna haja naye.

Nadhani pia ile ndoto ya kuwapo kwa shirikisho la nchi za Afrika Mashariki kwa maana ya kuungana kisiasa tuifute.

Hatuwezi kuungana kisiasa na kiuchumi na viongozi ambao wanaendesha nchi zao kihuni kihuni. Nadhani hatua tuliyoifikia ya kushirikiana katika ushuru wa forodha na mambo mengine yanatosha.

Watanzania kama tutajitia kimbele mbele cha kutaka kuungana na watu ambao hatuwajui vyema kama akina Museven ambao wanabadilika kama kinyonga, tutakuja kujuta.

Museven na uganda yake tuwaache waamue mambo yao na wakenya na Mwaki Kibaki wao tuwaache ugomvi wao wa ndizi na chungwa kuhusu katiba yao.

Tunajua wazi kuwa ingawa Tanzania tuna matatizo, lakini ya wenzetu Wanganda na Wakenya ni mazito zaidi.

Siamini kama rais wa Tanzania ajaye naye ataingia kucheza ngoma inayochezwa na Museven na Kibaki ya kutaka ushirikiano wa Afrika Mashariki bila kuelewa wenzake wanachezaje.

Kama ataingia kucheza ngoma asiyoijua ajue kuwa baada ya muda mfupi atapata matatizo makubwa ya ardhi, jeshi la watu wasiokuwa ajira na huenda watanzania wakakosa uvulimivu na kuingia mitaani kuandamana.

Alamsiki

Msabaha maafisa Tanesco kufanyakazi saa 24 kusimamia

WIKI hii Waziri wa Nishati na Madini, Dk. Ibrahim Msabaha aliwasha moto ndani ya Shirika la Umeme (Tanesco) kuwataka mabosi wa shirika hilo kuongeza muda wa kazi kwa ajili ya kusimamia ratiba ya mgawo wa umeme.

Kutokana na amri hiyo mameneja wa mikoa wa Tanesco wameamriwa kukaa ofisini hadi saa 2.00 usiku kufuatilia ratiba ya mgawo ili pale linapotokea tatizo wakati wa kurudisha umeme kwa watumiaji wadogo waweze kulishughulikia haraka.

Dk Msabaha ameuagiza uongozi wa Tanesco kuhakikisha makao makuu ya shirika kunakuwepo na maafisa saa 24 kupokea taarifa za watumiaji wa umeme.

Waziri anasema amelazimika kutoa maagizo hayo kuhakikisha umeme mdogo unaopatikana unagawiwa kwa haki na unatumiwa vizuri ili kukidhi mahitaji ya watumiaji wakubwa na wale wadogo.

Waziri Msabaha pia ameagiza makao makuu ya shirika hilo kuunda timu itakayosimamia na kufanya ukaguzi wa dharura kuona kama mgawo huo unatekelezwa na maafisa wa shirika hilo.

Nakubaliana na waziri Msabaha kabisa kuwa hivi sasa wakati wa mgawo wa umeme watu wote bila kubagua wanapaswa kupata mgawo sawa bila ya kuwepo upendeleo.

NI kweli pia kuwa nchi ipo katika matatizo makubwa ya ukame wa muda mrefu ambao umesababisha uzalishaji katika vyanzo vya umeme kupungua sana na hivyo kuzalisha umeme chini ya viwango kinachotakiwa.

Hata hivyo, uamuzi wa kulazmisha maafisa wa makao makuu ya TANESCO kukaa muda saa 24 ofisini kwa ajili ya kuangalia mgawo wa ume

Serikali kupitia Shirika lake la Umeme (Tanesco) limeanza kuachana na utegemezi nguvu za maji kama
chango umeme kwa kubuni vyanzo mbadala vitakavyozalisha umeme wa kutosha na kusaza.

Chini ya mpango huo muda mfupi na muda mrefu ambao utekelezaji wake umeanza mwezi huu, ifikapo Desemba
mwaka huu, shirika hilo litakuwa linapata megawati 528 za umeme bila kutegemea nguvu za maji, ikiwa ni
pungufu kidogo ya jumla ya umeme unaohitajika nchini wa megawati 560.

Mkurugenzi wa Uzalishaji Umeme wa Maji wa Tanesco, Declan Mhaiki, alithibitisha jana kuwepo kwa mpango
huo na kwamba tayari baadhi ya zabuni zimeshafunguliwa ili kuruhusu kuanza utekelezaji wake.

Hata hivyo, alisema sambamba na mpango huo, shirika halitaachana kabisa na umeme wa maji, lakini uwekezaji
katika umeme, hivi sasa utalalia katika vyanzo vingine, hasa gesi asilia ili kupata umeme wa uhakika,
badala ya huu wa kutegemea mvua za mashaka.

Mhaiki, alisema kwa sasa shirika lake linanunua umeme wote unaozalishwa na IPTL na Songas wa megawati 283 na
ifikapo Agosti mwaka huu, litakodisha mitambo ya dharura ya kuzalisha umeme wa kutumia gesi wa megawati
100. Zabuni zake zilifunguliwa Jumatatu iliyopita.

Alisema pia kuwa Tanesco Machi 13, mwaka huu ilifungua zabuni za kufunga mitambo ya kuzalisha megawati 60
nyingine za umeme wa kutumia gesi asilia katika kituo cha Ubungo na mingine ya megawati 40 katika kituo cha
Ilala, ambayo itakuwa tayari Desemba mwaka huu.

Chini ya mpango huo, Tanesco imedhamiria kuwa ifikapo Desemba mwaka huu, mitambo ya kuzalisha megawati 45
kwa kutumia gesi asilia iwe imefungwa Tegeta na kufanya umeme utakaozalishwa ndani ya mkakati huo
kufikia megawati 528, bila kuingiza umeme unaozalishwa na kwa nguvu za maji.

Katika mpango wake wa muda mrefu, Tanesco inakusudia kufunga mitambo mingine ya gesi asilia itakayofungwa
Kinyerezi Jijini Dar es Salaam ili kuzalisha megawati 200 ifikapo mwaka 2009 na baadaye kuunganisha gridi ya
Taifa na Zambia ili kununua megawati 200 zaidi za umeme ifikapo mwaka 2010.

Endapo mikakati hiyo itafanikiwa, ndani ya miaka mitano ya utawala wa Rais Jakaya Kikwete, Tanzania
itaweza kupata megawati 928 za umeme karibu mara mbili ya umeme unaohitajika nchini.

Akithibitisha kuwa umeme wa maji hajautupwa kabisa, Mhaiki, alimweleza Makamu wa Rais, Dk. Ali Mohamed
Shein, aliyetembelea bwawa la Mtera jana, kuwa ifikapo mwaka 2012 serikali itakuwa imejenga kituo kipya cha
kuzalisha umeme wa nguvu za maji katika mto Ruhdji kitakachozalisha megawati 358.

Mpango huo wa serikali umekuja baada ya kukosekana kwamatumaini katika umeme unaotegemea nguvu za maji hasa baada ya kukosekana kwa mvua kwa kipindi kirefu.

Mfano, bwawa la Mtera ambalo kwa hali yake ya kawaida huzalisha megawati 80, limekauka na kufikia katika
kiwango kisichoruhusiwa kutumika, lakini kwa kuwa majiyake baadaye hutumika kuzalisha umeme Kidatu mkoani
Morogoro, inabidi kuzalisha umeme usiozidi megawati 20 kwa siku ili kuruhusu maji kwenda Kidatu.

Hata mvua zinazoendelea kunyesha katika mikoa ya Dodoma, Mbeya na Iringa hazijaleta matumaini yoyote
kwani hadi jana maji yameongezeka kwa sentimita takriban 30, kufikia mita 687.68 tangu mwishoni mwa
Februari.

Mwenendo wa kupungua kwa kina cha maji hayo unatia shaka zaidi kwani kwa miaka mitano iliyopita, maji
yanayoingia bwawani humo yamepungua kutoka mita za ujazo 139 kwa sekunde mwaka 2001 hadi mita za ujazo 41
kwa sekunde mwaka jana.

Kwa mujibu wa meneja wa Kituo cha kuzalisha umeme cha Mtera, Nazir kachwamba, maji hayo mwaka huu yamefikia
kiwango cha chini kabisa ambacho hakikuwahi kufikiwa kwa miaka 20.

Mramba usilie, viatu vya
Magufuli vitakupwaya!

WIKI iliyopita Waziri Mkuu, Edward Lowassa alilazimika kumwita Waziri wa Miundombinu, Basil Pesembili Mramba mkoani Lindi kutoa maelezo kwa nini ujenzi wa barabara ya Lindi-Mingoyo haujakamilika kwa muda unaotakiwa.

Waziri Mkuu alifikia uamuzi huo baada ya kushangazwa na maendeleo ya ujenzi wa barabara hiyo ambayo yalionyesha wazi ni dhaifu.

Kulingana na mkataba wa ujenzi wa barabara hiyo, ilitakiwa ikabidhiwe serikalini na mkandarasi anayeijenga, kampuni ya AM Kharafi Oktoba 24 mwaka huu lakini hadi sasa hakuna hata sentimita moja ya barabara hiyo iliyokwisha wekwa lami.

Uamuzi huu wa kumwita Mramba kutoka Dar es Salaam kupanda ndege kumfuata waziri mkuu, ulitokana na Meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Lindi, Mwita Chacha kumweleza waziri mkuu kuwa, mkandarasi amevunja mkataba na kwamba hawezi kazi hiyo ya ujenzi wa barabara katika muda uliokubaliwa katika mkataba. Kutokana na hali hiyo, mkandarasi huyo alitakiwa kupigwa faini.

Mwita alisema pamoja na kuvunja mkataba huo hadi sasa, kampuni hiyo hajapigwa faini na serikali kutokana na sababu ambazo hazijui na kwamba kama ataachiwa kujenga barabara hiyo itachukua muda wa miezi 18 kuimaliza.

Hata hivyo, kampuni hiyo ya mkandarasi kutoka uarabuni inadaiwa kuwa ina matatizo na uongozi hali ambayo imechangia kushindwa kufanya kazi zake kwa ufanisi.

Hata hivyo, Waziri Mramba baada ya kuwasiliana mkoani Lindi akijieleza mbele wa waziri mkuu alilalamika kuwa, mkandarasi huyo amekuwa jeuri haambiliki na kwamba amekuwa akifanya kazi zake bila ya kufuata taratibu.

Alisema mbali ya wizara kumtaka akamilishe kazi zake haraka lakini amekuwa akikaidi agizo hilo na kwamba hata aina ya kokoto anazotaka kuzitumia katika ujenzi wa barabara hiyo haizifai.

Kwa hakika, kauli ya Mramba kuhusu mkandarasi huyo inatuchaganya sisi wananchi. Nasema inatuchaganya kwa sababu kama waziri aliyepewa dhamana ya kusimamia shughuli za barabara, analia kwa waziri mkuu sisi wananchi tufanye nini.

Tulitegemea kuwa Mramba angetueleza kwa nini wizara imeshindwa kumchukulia hatua ikiwamo kumsimamisha na kumtafuta mkandarasi mwingine.

Najua shughuli za kusimamia barabara ni ngumu kutokana na kuwa na fungu kubwa la hela ambalo linategwa kwa ajili ya ujenzi ambalo baadhi ya makandarasi wamekuwa wakilitumia kwa kushirikiana na wafanyakazi wa wizara kulitafuna.

Mramba anapaswa sasa kufahamu kuwa kwa kupewa wizara inayoshughulikia ujenzi na mawasiliano anatakiwa kukaza msuli kuhakikisha kuwa viatu vya waziri aliyepita katika wizara hiyo, John Pombe Magufuli katika kusimamia barabara vinamfiti, vinginevyo vitampwaya muda sio mrefu.

Kama mkandarasi anavunja mkataba, Mramba anapaswa kutupatia mkandarasi mwingine mwenye uwezo ili barabara zetu ziweze kukamilika kwa wakati. Kwa mwendo huu wa serikali kushindwa kuwachukulia hatua wakandarasi wanaovunja mikataba, ujenzi wa barabara unaoendelea nchini hivi sasa hautakamilika.

Ndoto iliyokuwapo mwaka 2003 kwa kiwango cha kupigiwa chapuo na rais mstaafu Benjamin Mkapa kuwa ifikapo mwaka huu kuwa mtu atasafiri kwa teksi kutoka Mwanza hadi Mtwara imeshindwa kutimia.

Kuna wakati niliandika katika safu hii kuwa ndoto hiyo haiwezi kutimia kutokana na kasi ya ujenzi iliyokuwa ikionekana kwa wakandarasi mbalimbali wanaojenga barabara zinazounganisha barabara hiyo. Lakini waziri Mramba alisema nilikuwa napigana serikali, nadhani sasa anaweza kukubaliana na mimi.

Wakandarasi wengi wanaojenga barabara zinazounganisha mtandao wa barabara hii bado hawafanyi kazi zao kwa ufanisi. Kwa mfano hivi majuzi tulisikia kuwa kampuni ya SIETCO kutoka China inayojenga barabara ya Igunga-Singida imeshindwa kukamilisha kazi yake kutokana na wabia katika kampuni hiyo kufilisika.

Meneja wa Mkoa wa Singida wa TANROADS, Paul Lyakurwa, alimwambia Makamu wa Rais, Dk Ali Mohamed Shein kuwa ujenzi wa barabara hiyo ulianza kusuasua Januari mwaka huu na baadaye ukasimama kabisa mwezi uliopita.

Mkandarasi huyo, amesimamisha kabisa shughuli zote za ujenzi wa barabara hiyo baada ya kujenga kilomita 18 tu za lami, kati ya kilomita 113.5 anazotakiwa kujenga.

Kutokana na hali hiyo, serikali ya China imeamua kutafuta wabia wengine ambao watakuja nchini kujenga. Kwa mifano hiyo inaonyesha wazi kuwa uteuzi wa makandarasi wa kujenga barabara bado sio mzuri huenda hauna chujio bora la kupata walio bora.

Kama utaratibu wetu ni mzuri ambao unaweza kutupatia wakandarasi walio bora basi, huenda utakuwa umegubikwa na rushwa kwa sababu barabara nyingi hapa nchini zimekuwa zikijengwa zaidi ya muda ambao mkandarasi amepewa na serikali.

Kikwete kwa hilo tuko pamoja

KUNA hadithi moja ambayo imekuwa ikisimuliwa tangu enzi ya mababu ya familia mbili ambazo zilikuwa na taratibu tofauti za kuishi.

Inasimuliwa kuwa kulikuwapo familia mbili zilizokuwa zikikaa pamoja moja ilikuwa ikiongozwa na baba mkali na nyingine ya mzee mpole.

Mzee Mkali katika familia yake aliweka masharti kadhaa kuhusu wageni waliokuwa wakija nyumbani kwake kutembelea. Mojawapo ya masharti ilikuwa ni wageni kutoingia chumba chake cha kulala, mgeni kubisha hodi kabla ya kuingia ndani, kutokula chakula kabla ya kukaribishwa na mgeni kutopata taarifa muhimu za kuhusu ulinzi wa nyumba..

Wakati familia ya Mzee Mkali ilijipatia heshima kubwa kutokana na msimamo huo, Mzee Mpole hakuweka masharti yoyote kwa wageni, kwa madia kuwa kuweka masharti kwa wageni ni ubaguzi na kinyume cha utamaduni wao. Wageni waliruhusiwa kuingia katika nyumba ya familia hiyo bila kuwekewa masharti. Waliruhusiwa kuingia kuanzia sebuleni na kutokea chumba cha kulala cha Mzee Mpole. Mgeni alifanya anachotaka bila ya kuulizwa.

Waliishi hivyo kwa miaka mingi, lakini ilitokea wakati familia hizo, zikagombana na kufikia kupigana vita. Familia ya Mzee Mpole ilishindwa vita kutokana na familia ya Mzee Mkali kuwa na mbinu nzuri za kivita ambazo hazikujulikana familia ya ya Mzee Mpole. Mzee Mkali alitumia upinde kuwarushia mishale na kuwaua maadui akiwa kwa mbali wakati Mzee Mpole na familia yake walitumia silaha duni za fimbo ambayo ziliwafanya washindwe kuua maadui.

Baadaye ilikuja kubainika kuwa Mzee Mkali alishinda vita kutokana na kujua adui yake anamiliki silaha za aina gani na akajiweka sawa.

Kwa nini Mzee Mkali alijua familia ya Mzee Mpole ina aina gani ya silaha? Ni kutokana na kukosa utaratibu wa kuigiza wageni ndani ya nyumba. Wageni kutoka familia ya Mzee Mkali waliingia mpaka chumbani na kuona aina ya silaha walizokuwa wanazo.

Kwa hakika mfano huo unafanana kabisa na hali ambayo ipo hapa nchini kuhusu utaratibu wa kukaribisha wageni.

Tanzania hivi sasa ni sawa na familia ya Mzee Mpole ambayo ina waachia wageni kuingia mpaka chumbani. Wageni hivi sasa wanaingia holela kufanya biashara na kazi bila hata ya kuulizwa na mtu.

Kauli ya mgombea urais wa CCM, Jakaya Mrisho Kikwete kuwa akifanikiwa kuingia madarakani serikali yake itapitia upya sera ya uwekezaji ili kudhibiti wimbi la raia wengi wa kigeni kuingia holale nchini na kufanya kazi, ni mwafaka na inafaa kuungwa mkono.

Kikwete akiwa katika kampeni zake za mwisho mwisho mkoani Morogoro wiki hii alisema lengo la serikali yake ijayo halitakuwa kukataza wageni kuja kuwekeza nchini, isipokuwa hawatakiwi kufanya kazi ambazo watanzania wanaweza kuzifanya.

Alitoa mfano kuwa kuna wafanyakjazi wengi wa kigeni katika hoteli za Ngorongoro na serena za mkoani Arusha na kazi wanazozifanya zinaweza kufanywa na watanzania.

Kwa hakika Kikwete kwa suala hilo naamini utawakuwa umewagusa watanzania wote. Hakuna nchi ambayo unaweza kuingia kihuni na kupata ajira bila ya kufuata taratibu.

Kutokana na upole wetu watanzania hivi sasa nchi yetu imekuwa ni eneo huru ambalo mtu yoyote anaweza kuingia na kufanua chochote bila hata mamamala zinazohusika kuhoji.

Kuna wageni hivi sasa wanafanya kazi za kuuza nyanya, pipi maua na hata karanga mitaani kwa mwavuli kuwa ni wawekezaji. Gazeti hili lilishawahi kuandika habari pamoja na kuchapisha picha ya Mchina ambaye alikuwa akiuza karanga eneo la Feri jijini Dar es Salaam.

Hivi kweli watanzania hawana uwezo wa kuuza karanga mpaka tumtafute mtalaam kutoka nje? Hivi kweli watanzania wamekosekana wa kulinda viwanda na migodi mpaka watafutwe watu kutoka Afrika Kusini na Cananda waje kufanya kazi hiyo?

Hivi kweli wasukuma, wakwele na wabondei hawawezi kuajiriwa kufweka majani ya uwanja wa ndege wa mwekezaji mpaka aajiriwe mtu kutoka uarabuni au Australia?

Kama watanzania tulikuwa familia ya Mzee Mpole sasa tuamke na kulinda nchi yetu na kwamba taratibu za kuruhusu wageni kuingia zifuatwe. Hivi sasa kutokana na kutokuwa hata na vitambulisho vya uraia sio rahisi hata kumtambua mtu asiyekuwa raia.

Mtu yoyote ambaye atafanikiwa kuingia madarakani, anapaswa pia kuingalia vyema idara ya uhamiaji. Idara hii imekuwa kibogonyo haina meno, hata pale inapokamata wageni baadhi wamekuwa baada ya siku mbili wanaonekana wanadunda mitaani. Tunafikiri kuna kasoro kubwa katika idara hii.

Kama tutaendelea na utaratibu huu, basi siku moja nchi hii haitakuwa na mwenyewe itakuwa ni ya wageni.

Kitu kingine ambacho ninaomba kumtahadharisha raia ambaye ataingia ikulu baada ya uchaguzi kuliogopa kama ukoma hiki kitu kinachooitwa shirikisho jipya la nchi za Afrika Mashariki.

Kama nilivyowahi kusema huko nyuma kuwa kuna wenzetu wanataka kutumia shirikisho hilo kutumia rasmali zetu, kumaliza matatizo ya ajira na ardhi na baadaye kutuacha hatuna kitu. Hawa watu hawataki shirikisho wana ajenda yao kibindoni.

Watanzania bado tuna kumbuka watu hawa wanaotaka shirikisho hili leo kwa uti na uvumba ndio hao hao walilikataa na kulivunja mwaka 1977.

Wapo watu kama akina Rais Yoweri Museven wa Uganda ameshatamka wazi kuwa anataka kuondoka madarakani baada ya kuundwa kwa shirikisho la Afrika Mashariki.

Inaonekana madaraka ya urais nchini mwake ambayo anayashikiliwa kwa nguvu zote anataka kuyatumia kama ngazi ya kufikia ndoto yake ya kuwa rais wa Afrika Mashariki. Watanzania tunasema hiyo ni itabaki ndoto tu!

Rais ajaye asikubali katika kuingia katika shirikisho hilo, ushirikiano wa nchi za Afrika Mashariki ubaki katika kushirikiana katika ushuru wa forodha na mambo madogo madogo kuzifanya nchi zetu kuwa nchi moja.

Ninajiuliza hivi tusipoingia katika shirikisho hilo tutapoteza nini?

Kikwete wala rushwa usiwape muda

WIKI hii Rais Jakaya Kikwete alisema anawajua kwa majina watumishi na watendaji wengine wa serikali wanaokula rushwa na kwamba alichofanya ni kuwaweka akiba ili wajisahihishe.

Alionya kwamba alikuwa hazungumzi kwa utani anajua anachosema na kwamba anapotembelea wizara na kuonya watumishi waache rushwa anawajua kwa majina.

Kikwete alisema kuawa anatoa muda kwa watu hao wajisahihishe na kwamba mwenye na asikie.

Rais Kikwete aliyasema hayo wakati akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika Uwanja wa Nelson Mandela mjini hapa, Rais Kikwete alisema mfanyakazi anayetekeleza kazi kwa kuzingatia maadili ya kazi yake, serikali inaweza kumtunuku nishani, lakini haitakuwa na muda na yule atakayekwenda kinyume.

Hata hivyo, alisema serikali haina ugomvi na mtu wala chuki ila inachotaka kutoka kwake ni utumishi wake uliotukuka.

Kwa hakika ninampogeza Rais Kikwete kwa kulizungumza tatizo la rushwa kwa uwazi na hata jitihada zake za kuwajua kwa majina vigogo wa rushwa katika sehemu mbalimbali za kazi nchini.

Nasema anafaa kupongezwa kwa sababu katika vita kitu muhimu ni kumfahamu adui yako kwanza yupo wapi na anasila zipi, kwa rais Kikwete hili tayari analijua halitamsumbua kitu.

Hata hivyo, ninadhani kuwa kwa vile rais Kikwete tayari majina anayo ya watu wanaojihusisha na rushwa hana haja kuwapa muda wa kujirekebisha aanze kuwashughulikia.

Kuwapa muda ni sawa na kuwapa muda wa kubuni mbinu nyingine ya kujihusisha na rushwa kwa njia ambayo inaweza kuwa mbaya zaidi.

Labda kitu cha kujiuliza ni kuwa hawa wala rushwa wameaanza kula rushwa lini? inawezekana kabisa wengine hivi sasa ni wazee ambao wamefanya kazi hiyo kwa muda mrefu na vitisho pekee vya serikali bila ya vitendo inawezekana pia vimeshazoeleka masikio mwao.

Nasema hivyo kwa sababu mapambano ya rushwa nchini yana historia ndefu sana. Nakumbuka awamu ya Kwanza ya Marehemu Mwalimu Julius Nyerere ilipambana vya kutosha kuhakikisha kuwa wala rushwa hawapati nafasi kupitia siasa ya azimio la arusha.

Hata hivyo, wapo wajanja waliotumia njia za ndani mchana waumini wa ujamaa usiku wanaendelea kula rushwa, ingawa inawezekana katika kiwango ambacho labda hakiweze kufananishwa na Tanzania ya leo.

Awamu ya pili ya Mzee Ali Hassan Mwinyi ilipoingia madarakani ilitangaza kuwa sasa inakuja na ufagio wa chuma wa kusafisha uchafu wote wote ikiwamo rushwa.

Kwa kwa siku za mwanzo wala rushwa hawa walitulia wakapima upepo unakwendaje ili waweze kubuni njia ya kuendelea na mchezo wao, na kwa bahati mbaya watu hawa baadaye waliendelea na mchezo bila matatizo.

Aamu ya tatu, ya rais mstaafu Benjamin Mkapa ilikuja mkakati wa kupambana na rushwa, hakuna mtu ambaye hakumbuki jinsi, Tume ya Jaji Warioba ilivyoibuka na ripoti iliyokuwa ikieleza mianya ya rushwa.

Serikali ikaapa kufa na wala rushwa, lakini baadaye nguvu za kupambana na rushwa taratibu zilianza kupungua na hatimaye tulishuhudia vigogo wawili au mmoja serikalini ndio walifikishwa mahakamani tu, waliobaki ni watumishi wa chini wa serikali waliopokea rushwa ya kuku au sh 3,000.

Kwa kuzingatia hitoria hiyo, tunadhani Mheshimiwa rais Kikwete anapaswa kuwachukulia hatua moja kwa moja badala ya kutoa muda wa kujirekebisha ambao hauana kikomo.

Rais Kikwete alitakiwa atoe muda wa kujirekebisha kwa watumishi hawa ambao unakikomo. Najua rais Kikwete ni mchapakazi ambaye kama alivyosema yeye mwenyewe amedhamiria kupambana na rushwa kikweli kweli.

Nadhani kutoa muda usio na kikomo ni kuwapa mwanya hawa wala rushwa kujiweka sawa kubuni mbinu nyingine za kuendeleaza ufisadi wao kwa vile wengi kama nilivyosema wapo ndani ya serikali yake tena wengine wapo katika nafasi ya kutoa maamuzi mazito ya nchi.

Ninapotafakari kwa kina ninadhani kuwa wala rushwa hawa wakubwa wamekuwepo karibu katika awamu zote za uongozi wa nchi uliopita na wakiendelea kuwadhurumu walala hoi, kuna haja gani kuwapa muda zaidi wakati ushahidi upo na wanafahamika?

Hivi kweli mtu tunamwona anakula rushwa ya kuifanya nchini kuingia mkataba ambao hauna maslahi ambao unaingizia serikali hasara ya mabilioni ya shilingi, huku tukijua kuwa alikupokea ten percent, tumwache ajirekebishe hadi lini?